BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

INSPEKTA HAROON KUACHANA NA MUZIKI ?, SASA KUJITUMBUKIZA RASMI FANI YA UCHEKESHAJI.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiK7Hnky2yGYiX2oCuFAnzlYtlzQA3chnHSw4sOWD18ip5fdi3_NGZ_3lIJ8rRT2LayoaFHzUXdphibV95F5M_XEuC442d-BsH2fVaXDJNMS2m5gnvkHeiOTqKwaRyztU98HnRGy5fTY7Ri/s400/nature.jpg 
UNALIKUMBUKA kundi la Gangwe Mobb, hapo lazima utamtaja Haruna Kaena ‘Insepkta Haroun’ na Luten Kalama, wawili hao baada ya kutengana kila mmoja akawa anafanya kazi binafsi lakini sasa Inspekta Haroun ameibuka na kudai kwamba anataka kuwa mwigizaji wa vichekesho.


Inspekta Haroun aliyetamba na wimbo wa ‘Mtoto wa Geti Kali’ aliendelea kueleza kwamba fani anazozipenda ni muziki na kuigiza vichekesho.


“Mimi msanii hivyo natakiwa niwe mbunifu, nisibweteke na kazi, fani moja na kwa sasa napenda kuwa mwigizaji wa vichekesho kwa kuwa napenda kazi hiyo na ninaiweza,” alijinadi.


Msanii huyo aliwahi kushirikishwa katika vipengele vya uigizaji katika kipindi cha vichekesho kilichokuwa kikirushwa na televisheni ya Clouds.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: