BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MGOMBEA URAIS WA UKAWA EDWARD LOWASSA ASHINDWA KUIBOMOA NGOME YA CCM BAADA YA KUSHINDWA KUHUTUBIA MIKUTANO YA KAMPENI YA LALA SALAMA KATIKA MAJIMBO MATATU MOROGORO.

Mwenyekiti wa NCCR-MAGEUZI wilaya ya Morogoro, Maulid Ibangi akihutubia mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Ukawa ambapo mgombea urais kupitia umoja huo Edward Lowassa ameshindwa kuwahutubia mamia ya wananchi waliojitokeza kutaka kumsikiliza uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege Manispaa ya Morogoro leo Okotba 23/ 2015.

Mgombea urais kupitia Ukawa Edward Lowassa leo ameshindwa kuhutubia mikutano miwili ya kampeni katika jimbo la Kilosa na Morogoro mjini kutokana na kubanwa na ratiba ya mikutano ya kampeni mkoani Morogoro.


Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara ulioandaliwa kwa ajili mgombea huyo wa nafasi ya urais, Mgombea ubunge wa jimbo la Morogoro Mjini Marcus Albanie aliwaelewa wanachama na wafuasi wa Ukawa katika uwanja wa Kiwanja cha Ndege kuwa Lowassa hawezi kufika katika viwanja hivyo kutokana na kubanwa na ratiba ngumu ya kampeni.


Albanie alisema kuwa Lowassa alitakiwa kuhutubia wananchi eneo hilo wakati akitokea Ifakara, Ruaha, Mikumi lakini ameshindwa na kuelekea Kibaha moja kwa moja.


Lowassa leo ameshindwa kuhutubia katika mikutano ya hadhara katika majimbo ya Mikumi, Kilosa na Morogoro.Chanzo.MTANDA BLOG
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: