BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

VITU VYA KUEPUKA SIKU YA JUMAPILI OKTOBA 25/2015 ILI USIINGIE MIKONONI MWA ASKARI POLISI.

 
Kujiepusha na vikundi vyenye muonekano wa kuzalisha vurugu.

Picha hizi zinatoka katika maktaba ya MTANDA BLOG na zilikuwa zikihusisha tukio la mmoja wa vijana kumzalilisha askari wa kike wa kikosi cha jeshi la zima moto na Uokoaji eneo la fire Manispaa ya Morogoro tarehe 10 juni 2015 baada ya kuanzisha vurugu kwa kufunga barabara ya mtaa wa Mindu na kusababisha kutotumika kwa masaa kadhaa.
Oktoba 25 mwaka 2015 ni siku ya kuweka historia kwa Tanzania ambapo wananchi wenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea hasa wenye sifa watapiga kura ya kumchagua kiongozi katika ngazi ya udiwani, ubunge na urais wa kuongoza nchi baada ya rais aliyepo madarakani kumaliza muda wake kulingana na matakwa ya katiba.

Jumapili ya Oktoba 25 ni siku ya kila mtanzania kuona siku hiyo ni muhimu kwake na yenye furaha lakini siku hiyo inaweza kugeuka chungu endapo mtu atajiingiza katika vurugu za namna yoyote na vyombo vya dola havitasita kuchukulia hatua za kinidhamu.
Vurugu hizo zinaweza kuzalishwa kwa mhusika endapo tu ataweza kutumia vilezi kama pombe, sigara haramu (bangi) ambapo vitu hivyo huchangia kumuondolea mtu akili zake za kufikili na kumpelekea kujiingiza katika mambo yanayopingana na sheria za nchi.

Hapa kuna matukio mbalimbali yanayoonyesha vijana waliovunja sheria za nchi lakini askari wenye thamana ya kutuliza ghasia wanaonekana wakiwadhibiti vijana hao.

Tukio hili ni tukio linalooonyesha vijana na askari wanavyoweza kutekeleza majukumu yao lakini askari hao wamekuwa na kawaida ya kuangalia nani amekuwa chanzo cha vurugu.

Hapo katika picha ya pili hadi ya nne anaonekana kijana ambaye alikuwa kinara wa vurugu hizo kabla na baada ya kumkamata na kumtia nguvuni.

Akili za kuambiwa changanya na zako, MTANDA BLOG inawatakiwa Tanzania wote siku ya jumapili Oktoba 25 tupige kura kwa amani na tusubirie matokea kwa njia iliyo ya utulivu ili kuendeleza amani iliyopo na siku hiyo isiwe siku ya kuanzisha vurugu, Mungu Ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.AMINA.

CHINI KUNA MUENDELEZO WA MATUKIO HAYO.













Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: