BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WANAJESHI WAFANYA KAZI YA ZIADA KUWAKOMBOA MATEKA 70 AMBAO WALIKUWA KATIKA MPANGO WA KUCHINJWA.

Islamic State
Image caption Wapiganaji wa Kikurdi wamekuwa wakijaribu kuwafurusha wapiganaji wa Islamic State maeneo ya Wakurdi

Wanajeshi wa Marekani wakishirikiana na wanajeshi wa Iraq wamefanikiwa kuwakomboa mateka 70 waliokuwa wakizuiliwa na wapiganaji wa Islamic State (IS) nchini Iraq.

Idara ya ulinzi ya Marekani imesema operesheni ya kuwakomboa mateka hao ilitekelezwa baada ya kubainika kwamba walikuwa karibu kuuawa.

Lakini mwanajeshi wa Marekani aliyejeruhiwa kwenye operesheni hiyo amefariki.

Ndiye mwanajeshi wa kwanza kufariki tangu kuanza kwa operesheni ya wanajeshi wa Marekani dhidi ya IS mwaka jana.

Kwenye operesheni hiyo iliyotekelezwa mapema Alhamisi karibu na mji wa Hawija kaskazini mwa Iraq, wapiganaji wa IS walinaswa na wengine kadha kuuawa, Pentagon imesema.

Jumla ya mateka 70 walikombolewa, maafisa wa ulinzi wamesema, wakiwemo Waarabu wa dhehebu la Wasunni, wanajeshi 20 wa Iraq na wanachama wa IS waliokuwa wakizuiliwa baada ya kushukiwa kuwa majasusi.

Hakuna watu wowote wa asili ya Kikurdi waliokombolewa, maafisa wa Pentagon na Wakurdi wamesema.

Habari za awali zilikuwa zimedokeza kwamba huenda kulikuwa na Wakurdi waliookolewa.

Wanajeshi wa Marekani walishiriki kwenye operesheni hiyo baada ya kupokea ombi kutoka kwa serikali ya jimbo lenye Wakurdi wengi Kirkuk.BBC
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: