BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SERIKALI YAKATA MZIZI WA FITINA KWA KUTENGA FEDHA SH 131.4 BIL KWA AJILI YA UENDESHAJI ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI

Serikali imetenga jumla ya shilingi  bilioni 131.4 kwa ajili ya kugharamia  uendeshaji wa  shule za msingi na  sekondari ili kuziba pengo la michango iliyokuwa ikichangishwa mashuleni.

Hayo  yamesemwa  na Waziri wa Nchi Ofisi  ya Rais-TAMISEMI ,Utumishi na Utawala Bora  Mhe. George Simbachawene  alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma jana.

Mheshimiwa Simbachawene alisema serikali imechukua jukumu  la kulipia michango  yote iliyokuwa ikitolewa na wazazi na walezi wa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ili kuziba pengo la michango hiyo.

Alisema dhana ya elimu bila malipo inazingatia uendeshaji wa shule bila ada wala michango yeyote  ya lazima kutoka kwa wazazi  au walezi wa wanafunzi.

Waziri Simbachawene alisema fedha zilizotolewa na serikali kwa ajili ya kugharimia elimu zitapelekwa moja kwa moja shuleni kutoka HAZINA kwa wastani wa shilingi bilioni 18.777 kwa ajili ya ruzuku za shule  kila mwezi.

Alifafanua kuwa ruzuku hizo za gharama za  uendeshaji wa shule ni shilingi 10,000 kwa wanafunzi wa shule za msingi na shilingi 25,000 kwa wanafunzi wa sekondari  kwa mwaka.

Alisema wanafunzi wa sekondari  wanaokaa shule za bweni  na  msingi watapata shilingi 1500 kwa siku ikiwa ni pamoja na fidia ya sh 20,000 kwa wanafunzi wa kutwa na sh. 70,000 kwa wanafunzi wa bweni kidato cha kwanza hadi cha nne.

Mheshimiwa Simbachawene alisema gharama za mitihani ya kidato cha nne zitalipwa na serikali moja kwa moja Baraza la Mitihani  hivyo wazazi na walezi hatawatawajibika kugharamia tena.

Naomba  ieleweke kwamba dhana ya elimu bila malipo haiondoi dhamira ya uzalendo kwa jamii kushiriki kwa hiari kuchangia michango katika kuleta maendeleo ya elimu hapa  nchini “alisema Mhe. Waziri

Mhe. Simbachawene alisema wazazi na walezi watawajibaka kununua sare za shule ,michezo, magodoro na mashuka ,vifaa vya usafi binafsi,vifaa vya kujifunzia vikiwemo madaftari,kalamu na chakula kwa wanafunzi wa kutwa.

Mahitaji mengine ambayo wazazi wanatakiwa kugharamikia ni matibabu kwa watoto wao,nauli za kwenda  na kurudi shule  kwa wanafunzi wa kutwa na kwa wanafunzi wa bweni wakati wa likizo.

Wakati huo katika taarifa iliyotolewa kwa niaba ya Waziri huyo  na Mkuu wa  Kitengo cha MawasilianoSerikalini wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI Bibi Rebecca Kwandu,  ilisema kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. George Simbachawene amemwagiza mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma kuwasimamisha kazi mara moja Kaimu Afisa Biashara Bw.Elias Kamara  na Afisa Biashara Bibi Donatila Vedastokutokana na makosa waliyoyafanya katika utendaji wao wa kazi.

Alitaja sababu za kusimasishwa kwao kuwa ni kutokana na kuisababishia hasara manispaa hiyo ya jumla ya shilingi  milioni 75 kutokana  na  urasimu wa utoaji leseni za biashara.

Alisema katika uchunguzi uliofanywa  katika halmashauri hiyo ya Manispaa ya Dodoma imegundulika kuwa kulikuwa na maombi 750 ya leseni ambayo  yalikuwa hayajashughulikiwa bila sababu za msingi.

Alisema mhe. Simbachawene ameagiza watumishi hao wachukuliwe hatua za kinidhamu wakati ikiwepo kusimamishwa kazi wakati uchunguzi dhidi yao ukifanyika.chanzo:Mzee wa Matukio.

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: