Juma Mtanda, Morogoro.
Timu ya soka ya
Kinglwira FC imeishushia mvua ya mabao Kihonda Star katika muendelezo wa
ligi daraja la nne msimu wa mwaka 2015/2016 kwa kuicharaza bao 3-0
katika mchezo mkali uliofanyika jana kwenye uwanja wa Sabasaba mkoani
Morogoro.
Mshambuliaji wa Kinglwira FC, Nurdin Nurdin ndiye
aliyeonekana mwiba mchungu kwa timu ya Kihonda Star kwa kufunga bao
mbili pekee katika dakika ya 82 na 90 kufuatia pasi za mwisho za
wachezaji Mohamed Mnyepe na Salum Nzange.
Nurdin alifunga
mabao hayo moja akifunga kwa tiktaka baada ya mpira wa kona ulioanzishwa
na Omari Godfrey kisha kukumiminwa krosi iliyomkuta mfungaji kabla ya
kupokea pasi ya Salum Nzange.
Bao la kwanza la Kinglwira
lilifungwa na Mohamed Mnyepe dakika ya 43 huku Kihonda Star ikishindwa
kufurukuta mbele ya wapinzani wao katika mchezo huo.
Katika
michezo mingine timu ya Moro Youth FC ilitembeza kipigo kwa timu ya
G-Seven baada ya kuisambaratisha kwa bao 4-1 wakati Don Bosco FC na
Uluguay ya Sultan zikishindwa kutambiana baada ya sare ya bao 1-1.
Timu ya Maskan FC yenyewe ilikubali kutandikwa bao 1-0 mbele ya Barafu
FC ya Kihonda na Magadu FC na Lubungo FC zilishindwa kucheza mchezo wao
Desemba 26 ikipisha ligi daraja la kwanza kwa mchezo baina ya Polisi
Moro SC na Burkina katika mchezo uloisha kwa sare ya bao 2-2.
Katika
mchezo huo kati ya Magadu FC na Lubungo FC utachezwa januari mosi
ambapo katika mchezo wa leo (jana) Moro City FC itaonyesha umwamba na
Chipolopolo FC saa 10 jioni katika uwanja wa Sabasaba.CHANZO:MTANDA BLOG
MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO
Home / michezo /
slider
/ TIMU YA SOKA YA KINGLWIRA FC YASHUSHA KIPIGO KIKALI KWA KIHONDA STAR MORO.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)

0 comments:
Post a Comment