BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

ZOEZI LA KUSAKA MIILI AJALI YA KUPINDUKA KWA KIVUKO CHA MV II KILOMBERO YAKUMBWA NA CHANGAMOTO MOROGORO

Na Juma Mtanda, Kilombero.
Zoezi la kusaka miili ya abiria katika ajali ya kupinduka kwa kivuko cha MV II Kilombero limeonekana kukubikwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ugumu wa kuopoa kivuko kutokana na ongezeko kujaa na  kasi ya maji katika mto Kilombero mkoani Morogoro.

Akizungumza na wandishi wa habari eneo la kivuko cha mto Kilombero, Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa) Mhandishi Margreth Mapela alisema kuwa ugumu wa zoezi la kukiopoa kivuko cha MV11 Kilombero na kupata maiti kutokana na ongezeko la kujaa na  kasi ya maji katika mto huo.

Mapela alisema kuwa baada ya kukumbwa na changamoto hizo, tayari gari la kunyanyua vitu vizito (Clean ya Temesa) pamoja na lile la kampuni ya ujenzi ya daraja la kudumu la mto huo vimefika eneo la tukio ili kuweza kufanya kazi ya kuopoa kivuko hicho.

“Kuna ugumu wa zoezi la kuopoa kivuko cha MV II Kilombero na kuangalia kama kuna uwezekano wa kupata maiti kama watakuwa wamekwama katika kivuko.”alisema Mapela.

Mapela alisema kuwa tayari kikosi cha JWTZ kimewasiri jana (juzi) na kuanza kutoa huduma za kuvusha watu na wengine wakiendelea na kazi ya kukiibua kivuko kwa kushirikiana na  kampuni ya M. Divers Ltd ya Dar es Salaam ambapo watalaamu wao wamefanikiwa kuokoa baiskeli mbili na zoezi hilo linaendelea.

Lengo lao kuzamia wataalamu hao ni kuanza kuchunguza kisha kuweka maboya ambayo yatafanikisha kukiibua kivuko hicho na hatua itayofuata ni kukivuta na kukitoa nchikavu.

Wakati watalaamu wa kampuni ya M. Divers Ltd wakishirikiana na Temesa, JWTZ katika kukiibua kivuko cha mto Kilombero, watalaamu wengine wa kampuni ya May-Marine Go Ltd wamekuwa na kazi ya kutafuta magari ili kuyaibua.

Mkurugenzi wa M. Divers Ltd, Salvatory Murungi alisema kuwa uwepo wa eneo hilo umetokana na kuongeza nguvu katika kazi za kuibua magari likiwemo la benki ya CRDB inayodhaniwa ndani ya gari yake kuwa na mtu na magarin mengine mawili.

Murungi alisema kuwa kazi iliyopo mbele yao leo (jana) ni kuanza kazi ya wazamiaji wake kuzamia majini kutafuta gari hazi chini ya maji na baada ya kuonekana yatafungwa maboya ili yaweze kuibuka yenyewe na kufunga kamba kuyatoa nchikavu.

Kutokana na kivuko cha MV II Kilombero kupinduka januaria 25, kumejitokeza na mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali katika baadhi ya wilaya ya Ulanga.

 Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu, Diwani wa kata ya Isongo wilaya ya Ulanga, Henry Barua alisema kuwa baadhi ya wafanyabiashara wametumia mwanya wa kukosekana kwa huduma za kivuko hicho, kumekuwa na mfumuko wa bei wa bidhaa muhimu.

Barua alisema kuwa baadhi ya wafanyabiashara wilaya hiyo wametumia mwanya huo kupandisha bei ya bidhaa muhimu kufuatia kivuko hicho kupinduka.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: