BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

NEEMA ALIYOKUMBANA NAYO BONDIA FRANCIS CHEKA YAWAANGUKIA BASIL MRAMBA NA DANIEL YONA.

Mawaziri wa zamani wakati wa awamu ya Tatu, Basil Mramba (Waziri wa Fedha) na Daniel Yona (Nishati na Madini) sasa kutumikia kifungo cha nje hadi Novemba 5 mwaka huu kwa kufanya usafi wa mazingira katika Hospitali ya Palestina Iliyopo Sinza.

Ikumbukwe Julai 6, 2015 mawaziri hao walihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela na kulipa faini ya milioni tano kila mmoja kwa kosa la matumizi mabaya ya madaraka na kuisababishia serikali hasara.

Adhabu kama hiyo imewahi kumkuta bondia wa ngumi za kulipwa Francis Cheka ambaye naye alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela kwa kosa la kumpiga Meneja wake ngumi lakini baadaye aliweza kubadilishiwa adhabu na
kutumikia kifungo cha nje kwa kufanya usafi eneo la kituo cha Zimamoto mkoa wa Morogoro.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: