BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SAUTI YA WANANCHI JUU YA BAJETI YA SERIKALI YA MWAKA 2016/2017 ILIYOSOMWA NA WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO.

IRENE KOMBA.
 Mfano kodi ya vat ya 10% ya utumaji wa fedha katika simu kwenda kwa mpokeaji inaumiza pande zote mbili ila mtu wa mwisho ndiye anayeumia zaidi.

Ikipitishwa hiyo bajeti mtu wa kijijini ndiye atayeumia zaidi kwani atalazimika makampuni ya simu kumkata zaidi ya asilimia 10 maana katika kupokea fedha kutoka mtumaji atakatwa asilimia na wakati wa kutoa fedha hizo atakatwa tena asilimia, naona serikali imekuja katika kumkandamiza mwananchi wa kawaida tu.
BONINVETURE MTALIMBO.
 
Nimevutiwa na bajeti ya mwaka 2016/2017 ya kuwata wabunge kuwa sehemu ya viongozi wa Tanzania kuwajibika katika kulipa kodi kwani wao ni sehemu ya wananchi na kuwa  wanapaswa kuonyesha mfano  kwa wananchi katika uwajibikaji wa kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo  ya Nchi.
Mpango huo ukitekeleza utakuwa sehemu ya ukusanyaji wa mapato kwani wamekuwa wakiingiza kipato kikubwa ambacho kimekuwa hakilipwi kodi na serikali kupoteza mapato kutoka kwenye kundi hilo na wengine.

MDINI MOHAMED MSUMI (46).
 
Bajeti iliyosomwa na waziri wa fedha na mipango hasa sekta ya fedha iendeleza kuwaminya kiuchumi wananchi wa kawaida hali itayopelekea kuongezeka ugumu wa maisha badala ya kupunguza makali ya maisha yaliyo sahihi.
Suala ya kutoza kodi ya vat katika simu kwa mpokeaji na mtumiaji niishauri serikali iondolewe kabisa kwani nia ya serikali ni kumpunguzia machungu mwananchi wa kawaida, mimi naona serikali ijikite zaidi katika ukusanyaji kodi katika makampuni makubwa kama sekta ya madini, bandari na kusiwepo misamaha ya kodi kwa makampuni hapo.
 
REHEMA MKWAMA.
 
Bajeti ya mwaka 2016/2017 ya 9% ambayo serikali imepunguza kutoka asilimia 11 ambayo mfanyakazi analipa malipo yake (P.A.YE) haimsaidii mlengwa.
Kwa sababu 9% ni fedha ndogo sana ukilinganisha ongezeko la fedha katika mshahara kwani mahitaji halisi ya maisha bado inamuumiza mfanyakazi, imeandaliwaa na MTANDA BLOG.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: