BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

TASWIRA ZA MATUKIO MANISPAA YA MOROGORO JULAI 17/2016.

Askari kata ya Uwanja wa taifa Manispaa ya Morogoro, Mbaraka Mahanyu kulia na afisa ustawi wa jamii wa kata hiyo kushoto wakimpeleka mkazi wa mtaa wa Kiswanya B, Farida Ghumpi (34) kituo cha polisi baada ya kudaiwa kumtumikisha mwanafunzi wa shule ya msingi Mwau kijiji cha Ikungi Singida anayedaiwa kusoma darasa la tano, Shaminu Iddi (12) kazi za ndani, kabla ya kitengo cha dawati la jinsia cha jeshi polisi kumwamuru kumlipa mtoto huyo stahiki zake ikiwemo kiasi cha Sh75,000 kisha kumrudisha kijijini kwao.
Mafundi selemala katika kalakana iliyopo eneo la Fire kata ya Sabasaba Manispaa ya Morogoro wakiendelea na kazi ya kutengeneza madawati yanayotarajiwa kutumiwa na wanafunzi, mkoa wa Morogoro una upungufu wa madawati 73,972 kwa shule za sekondari na msingi.PICHA ZOTE NA MTANDA BLOG



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora , Angela Kairuki akizungumza jambo na watumishi mbalimbali wa idara za serikali katika ukumbi wa Manispaa ya Morogoro, kushoto ni Mkuu wa mkoa huo, Dk Steven Kebwe na kulia ni mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina ChonjoMmoja wa watumishi akitoa kero kwa waziri
Baadhi ya wakuu wapya wa wilaya za mkoa wa Morogoro kutoka kushoto, Siriel Mchemba (Gairo), Regina Chonjo (Morogoro), Mohamedi Utaly (Mvomero) na Jacob Kassema (Ulanga) wakimsikiliza mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Steven Kebwe (hayupo pichani) wakati akitoa taarifa juu ya kuwepo kwa watumishi hewa 315 huku wilaya ya Kilosa ikiongoza kwa kuwa na watumishi hewa 98 na zoezi la utengenezaji wa madawati ulioagizwa na rais John Magufuli.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: