BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SHEREHE ZA HARUSI ZAPIGWA MARUFUKU

Sherehe za usiku
Mamlaka katika mji wa pwani ya Kenya, Mombasa imepiga marufuku harusi za usiku kutokana na sababu za kiusalama.

Kamishna wa eneo hilo Maalim Mohammed anasema kuwa hatua hiyo inalenga kuwalinda wakaazi dhidi ya mashambulio ya magenge yanayotumia visu.

Magenge hayo yamekuwa tatizo kubwa kwa wakaazi katika siku za hivi karibuni huku baadhi ya wakaazi wakiripoti kushambuliwa wakati wa mchana .

Maafisa wa polisi wamekuwa wakifanya operesheni za kiusalama huku washukiwa kadhaa wa magenge hayo wakiuawa.

Wakaazi wa pwani hufanya sana harusi za usiku ambazo huendelea kwa takriban siku kadhaa ikiwemo sherehe za usiku.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: