BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

SIMBA SC YAWA NGUZO UFUNGUZI LIGI KUU TANZANIA BARA 2016/2017 BAADA YA KUANZA KWA KISHINDO DHIDI YA NDANDA FC.

SIMBA imeanza kwa kishindo Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Ndanda FC ya Mtwara katika mchezo uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mabao yote ya Simba yaliwekwa kimiani na wachezaji wake waliosajiliwa katika dirisha la usajili lililomalizika hivi karibuni.

Ushindi huo umeifanya Simba kuondoka na pointi tatu muhimu na kupeleka raha kwa mashabiki wa timu hiyo, ambao kwa miaka kadhaa walikosa raha kwa timu yao kufanya vibaya.

Mshambuliaji mpya wa Simba, Laudit Mavugo alifunga katika dakika ya 19 baada ya kuunganisha mpira wa adhabu uliopigwa na Mohamed Hussein `Tshabalala’.

Hatahivyo, Omary Mponda wa Ndanda aliisawazishia timu yake kwa bao la dakika ya 36 kwa kichwa akiunganisha wavuni mpira wa adhabu uliopigwa na Kiggy Makassy.

Simba walizidi kukaribia ushindi baada ya kupata bao la pili lililofungwa na mchezaji wake wa Ivory Coast, Frederic Blagnon aliyeingia akitokea benchi kuchukua nafasi ya Mohamed Ibrahim.

Wekundu hao wa Msimbazi walijihakikishia ushindi baada ya kufunga bao la tatu kupitia kwa Shiza Kichuya katika dakika ya 74 baada ya kuunganisha mpira wa kona uliokolewa na kurudi uwanjani na kumkuta mfungaji aliyechia kiki kali.

Kikosi Simba: Vicent Angban, Malika Ndeule, Mohamed Hussein, Method Mwanjale/Mwinyi Kazimoto, Juuko Murshid, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Mohammed Ibrahim/ Frederic Blagnon, Laudit Mavugo, Ibrahim Ajib na Jamal Mnyate.

Katika mchezo mwingine; Ruvu Shooting iliifunga Mtibwa Sugar bao 1-0 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Manungu Turiani.

Nayo Stand United ilitoka suluhu na Mbao FC katika mchezo mwingine wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga.

Prisons imeondoka na pointi zote tatu baada ya kuidungua Majimaji ya Songea katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: