BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

FREEMAN MBOWE ADONDOSHWA CHINI NA KUANGUKIA PUA



MAHAKAMA Kuu ya Tanzania imetupilia mbali maombi ya Mfanyabiashara na Mwanasiasa, Freeman Mbowe, kutaka kurudishwa kwenye jengo la Bilicanas, baada ya kuondolewa na Shirika la Nyumba la Taifa kwa kudaiwa kodi ya Shilingi bilioni 1.3.


Akitoa uamuzi huo leo asubuhi, Jaji Sivangilwa Mwangesi alisema kuwa Mahakama imechukua uamuzi huo baada ya kujiridhisha na hoja kuu tatu kuwa hakuna mkataba wa ubia uliopo baina ya NHC na Mbowe Hotels Limited na kuwa mahusiano pekee yaliyosalia ni ya Mpangaji na Mpangishaji.


Pia Jaji Mwangesi amesema kuwa Mahakama imejiridhisha kuwa NHC imefuata taratibu zote katika kuiondoa Mbowe Hotels Limited kwa kutoa ilani ya siku 30 na baadaye siku 14 kabla ya kumtoa mteja wao huyo.


Kuhusu kusajiliwa au kutosajiliwa kama dalali rasmi wa Mahakama wa kuendesha mchakato wa kumhamisha Mbowe katika jengo hilo alisema hiyo nayo haikuwa hoja yenye mashiko na kwamba waombaji walitakiwa kuwasiliana na Msajili wa Mabaraza ya Ardhi.


NHC katika shauri hilo iliongozwa na Wakili Kiongozi, Aloyce Sekule na Ipilinga Panya na mawakili wengine wa Shirika waliojikita katika kujibu hoja zilizokuwa zikitolewa na wateja wao
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: