BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

PICHA TANO ZA KUNUNIANA KATI YA RAIS OBAMA NA RAIS MTEULE TRUMP KATIKA IKULU YA MAREKANI

Trump na Obama wakiwa Oval OfficeRais mteule wa Marekani Donald Trump alipokutana na Rais Barack Obama kwa mara ya kwanza ikulu ya White House tangu ashinde uchaguzi, uadui kati yao ulijidhihirisha.

Trump kwenye kampeni alimweleza Obama kama rais mbaya zaidi kuwahi kuongoza Marekani.

Rais Obama naye alisema Mwanarepublican huyo hana sifa na uwezo wa kuwa kiongozi wa Marekani.

Mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York, ambaye sasa ni rais mteule, kwa muda mrefu alitilia shaka uhalali wa habari kwamba Obama alizaliwa Hawaii, na alikejeliwa hadharani na Rais Obama.

Wawili hao walishauriana kwa zaidi ya saa moja afisi ya rais katika ikulu ya White House mnamo Alhamisi na walipojitokeza kwa wanahabari, walijaribu kuficha uadui kati yao.

Waliongea maneno mazuri kuhusu umoja na umuhimu wa kupokezana madaraka kwa amani lakini picha zilizopigwa zinaonesha jambo tofauti, ukiangalia sura na mikono.Trump na Obama wakiwa Oval OfficeNikiangalia sana pale mbali, haya masaibu yote yatapita.Trump na Obama wakiwa Oval OfficeFikira za Trump zinaonekana kuyumba.... labda kwa kukumbuka aibu iliyotokana na utani kuhusu kuzaliwa kwa Obama mwaka 2011. Trump na Obama wakiwa Oval OfficeWanasalimiana lakini macho yako wapi.... tazama mdomo wa Trump Trump na Obama wakiwa Oval OfficeTena, sasa Obama anamwangalia Trump.... lakini Trump anaamua, la hasha, SIWEZI kumwangalia machoniTrump na Obama wakiwa Oval OfficeKupeana mikono kwisha sasa, na ni furaha sana kwa Trump .... lakini anaonekana kutoyaamini anayoyasema Rais Obama Trump na Obama wakiwa Oval OfficeWawili hao walicheka wakati mmoja walipotaniana. 

Melania na Michelle pia walikutana, lakini hawakuonekana kuwa na matatizo
Melania Trump na Michelle ObamaMelania Trump na Michelle Obama wakiwa ikulu ya White House.BBC
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: