BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

TRUMP ACHUKIZWA NA UHESABUJI WA KURA UPYA MAREKANI


Rais Mteule wa Marekani, Donald Trump, ametaja mipango ya kuhesabu kura upya katika jimbo la Wisconsin kama kashfa.

Alisema kuwa hata mpinzani wake mkuu Hillary Clinton amekubali matokeo ya uchaguzi.

Bwana Trump alimshinda Bi Clinton kwa kura chache sana katika Wisconson lakini chama cha Green Party kimeomba rasmi kura hizo zihesabiwe tena ili kuhakikisha kuwa hakuna magendo yoyote yaliyofanywa.

Bwana Trump alisema kuwa kiongozi wa Green Party, Jill Stein, anajaribu kurejesha pesa alizopoteza wakati wa kampeni kwa kisingizio kuwa anataka kura kuhesabiwa upya.

Chama hicho pia kinakusudia kuchochea shughuli za kuhesabu kura upya katika majimbo ya Pennsylivania na Michingan.

Msemaji wa Bi Clinton alisema kuwa shughuli za kuhesabu upya kura zikianza, kundi lake litashiriki.

Lakini wachunguzi wa kisiasa wanasema kupunguza kura katika majimbo yote matatu ni jambo ambalo si rahisi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: