BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WANAWAKE WAWILI WAKAMATWA NA KILO 114 ZA MADAWA YA KULEVYA MWANZA


Mwanza. Wanawake wawili ni miongoni mwa watu zaidi ya 15 waliokamatwa kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya mkoani Mwanza

Watu hao wamekamatwa wakijihusisha na dawa hizo ndani ya wiki moja kuanzia Febuari 6.

Habari zinasema wanawake hao wamekamatwa wilayani Magu wakiwa na kilo 114.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi amesema watuhumiwa 11 wamekamatwa wilayani Nyamagana na Ilemela na kilo 57 za dawa za kulevya aina ya miraa na kete mbili zinazodaiwa kuwa ni heroin.

“Mtuhumiwa mwingine ambaye ni mfanyabiashara wa vipuri vya magari, alikamatwa eneo la Butimba akiwa na kete 240 ya dawa za kulevya zinazodaiwa kuwa ni heroin na ndunga mbili,” amesema.


Msangi amesema mtuhumiwa huyo alitaka kuzitumbukiza chooni dawa hizo ili kupoteza ushahidi, lakini polisi waliwahi kukata bomba.mwananchi
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: