BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MLINZI WA SHULE YA SEKONDARI AFUNGWA MIAKA 30 BAADA YA KUMBAKA MTOTO WA MIAKA 16


Mahakama ya Wilaya ya Mlele imemuhukumu mlinzi wa Sekondari Ilela, George Sikoki kutumikia kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mtoto wa umri wa miaka 16.

Hukumu hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Hakimu Mkazi Mfawidhi Teotimus Swai baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa.

Mwendesha mashtaka, Baraka Hongoli alidai katika ushahidi mahakamani hapo kuwa, mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 27 saa 7:30 usiku.

Alidai Sikoki ambaye ni mlinzi wa shule hiyo iliyopo tarafa ya Inyonga wilayani hapa alitenda kosa hilo wakati ambao wazazi wa mtoto huyo wakiwa safirini naye alikuwa akilala peke yake.

Upande wa mashtaka ulidai mshtakiwa alikwenda nyumbani kwa mtoto huyo na kuvunja mlango kisha kumtishia kumuua iwapo angepiga kelele hivyo kumbaka na kutokomea kusikojulikana.

Ilielezwa mahakamani kuwa binti huyo akiwa na maumivu makali, huku akitokwa damu sehemu za siri alijikongoja hadi kwa jirani na kutoa taarifa ndipo alipopelekwa hospitali kwa matibabu.

Hongoli alidai baada ya mshtakiwa kukamatwa alikiri kosa hilo kwa maandishi wakati akihojiwa kituo cha polisi, lakini alipofikishwa mahakamani alikana. 


Upande wa mashtaka ulipeleka mahakamani mashahidi sita akiwamo daktari kuthibitisha shtaka hilo ambapo waliithibitishia mahakamani bila kuacha shaka.Mwananchi
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: