BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

REAL MADRID YAICHAKAZA JUVENTUS MCHEZO WA FAINALI KOMBE LA LIGI YA MABINGWA ULAYA BAO 4-1, RONALDO AIBUKA SHUJAA

Klabu ya Real Madrid ya Uhispania imeicharaza Juventus ya Italia 4-1 na kushinda Kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Mreno Cristiano Ronaldo alifunga mabao mawili, la kwanza kwake na klabu dakika ya 20 na lake la pili dakika ya 64 kutoka kwa krosi ya Luka Modric.

Casemiro aliwafungia Real bao lao la pili dakika ya 61 kabla ya Marco Asensio kukamilisha ushindi wao dakika ya 90 kwa bao lao la nne.

Juventus, waliokuwa wameanza vyema mechi hiyo wakikuwa wamekomboa bao la kwanza la Ronaldo dakika ya 27 kupitia Mario Mandzukic na kufanya mambo kuwa sare wakati wa mapumziko lakini kipindi cha pili mawimbi yaliwageuka.

Nguvu mpya wao Juan Cuadrado alipewa kadi ya pili ya manjano dakika ya 84, baada ya kukaa uwanjani dakika 18 pekee.

Gareth Bale aliingia kwenye mechi hiyo kama nguvu mpya dakika ya 77, mara yake ya kwanza kuchezeshwa mechi ya ushindani tangu 23 Aprili.

Mechi hiyo iliyochezewa Cardiff ilikuwa ya 19 kwa klabu hizo mbili kukutana, mechi zote zikiwa katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya/Kombe la Ulaya.

Klabu hizo ndizo zilizokutana mara nyingi kabisa historia ya michuano hiyo, baada ya Bayern dhidi ya Real Madrid (24).

Juventus na Real Madrid, kila mmoja alikuwa ameshinda mechi nane kati ya hizo, mechi mbili zikimalizika kwa sare.

Mechi yao pekee kukutana fainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, Real walishinda 1-0 mwaka 1998 kupitia bao la Pedrag Mijatovic.

Juventus walikuwa wameshinda mara mbili pekee kati ya fainali nane walizocheza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya/Kombe la Ulaya. Walishindwa fainali nne walizocheza karibuni zaidi mwaka 1997, 1998, 2003 na 2015.

Real Madrid wamefanikiwa kuwa klabu ya kwanza tangu AC Milan (1989, 1990) kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya/Kombe la Ulaya misimu miwili mfululizo, na ni mara yao ya 12 kushinda kombe hilo.

Mwaka huu ni mara ya tatu kwa Real Madrid kufika fainali katika misimu minne.

Juve ndiyo klabu pekee ambayo ilikuwa haijashindwa mechi yoyote msimu huu Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, klabu ya kwanza tangu Atletico Madrid mwaka 2013/14 kufika fainali bila kushindwa.

Real Madrid nao walikuwa wamefunga kila mechi kati ya mechi 12 walizocheza Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu huu.

Kushindwa kwa Juventus ni pigo kubwa kwa nahodha wao, mlinda lango Gianluigi Buffon, 39, ambaye hajawahi kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Kabla ya mechi, alikuwa amesema ushindi ungekuwa na maana kubwa sana kwake.

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: