BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KASUKU AFICHUA MAUAJI BAADA YA MWANAMKE KUMUUA MUMEWE KWA KUMPIGA RISASI

Kasuku sawa na huyu ana uwezo mkubwa wa kuiga sauti

Mwanamke amepatikana na hatia ya kumuua kwa kuimpiga risasi mumewe mara tano katika jimbo la Michigan kwenye kisa ambacho kilishuhudiwa na kasuku.

Glenna Duram alimpiga risasi mumewe mbele ya kasuku huyo mwaka 2015 na kisha akajaribu kujiua kwa kujipiga risasi.

Kasuku huyo anayejulikana kama Bud, baadaye alirejelea maneno "usipige risasi" kwa sauti ya muathiriwa, kwa mujibu wa mke wa zamani wa Duram. Glenna Duram amepatikana na hatia ya kumuua mumewe Martin

Hata hivyo kasuku huyo hakutumiwa wakati wa kesi mahakamani.

Jaji alimpata Bi Duram 49, na makosa wa mauaji na atahukiwa mwezi ujao.

Alipata majeraha ya kichwa wakati wa kisa hicho kilichotokea nyumbani kwao mwezi Mei mwaka 2015.

Mke wa zamani wa Duram Christina Keller, ambaye sasa anamiliki Kasuku Bud, mapema alisema anaamini chiriku huyo alikuwa akirejelea mazungumzo ya kutoka usiku wa mauaji ambayo anasema yaliishia kwa kusema "usipige risasi".BBC
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: