BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WANAUME WAPUNGUKIWA NA MBEGU ZA KIUME, BINADAMU WAPO SHAKANI KUTOWEKA DUNIANI MIAKA IJAYO.

Watafiti wanaochunguza matokeo yao tafiti 200 wanasema kuwa upungufu wa kiwango cha mbegu za kiume miongoni mwa Wanaume kutoka Marekani kaskazini, Ulaya, Australia na New Zealand ufikia nusu yake.

Baadhi ya wataalam wanashaka kuhusu matokeo hayo.

Lakini mtafiti bingwa anayeongoza utafiti huo Dkt Hagi Levine anasema kuwa alikuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu kile kitakachofanyika katika siku za usoni.

Dkt. Levine ambaye ni mtaalamu wa magonjwa aliambia BBC kwamba iwapo mwenendo huo utaendelea basi huenda binadamu wakatoweka.

Utafiti huo ambao ni miongoni mwa tafiti kubwa ulileta matokeo ya tafiti 185 kati ya 1973 na 2011.

''Iwapo hatutabadili mienendo yetu ya kuishi mbali na kemikali na mazingira yetu ,nina wasiwasi mkubwa kuhusu kile kitakachofanyika siku za usoni''.

Hatimaye tutakuwa na tatizo hususan na uzazi kwa jumla na huenda ikawa kutoweka kwa binaadamu.

Wanasayansi ambao hawakushirikishwa katika utafiti huo wameusifu ubora wake lakini wanasema kuwa huenda ni mapema mno kutoa tangazo hilo.

Dkt. Levina kutoka chuo kikuu cha Hebrew mjini Jerusalem alibaini kupungua kwa asilimia 52.4 ya manii huku asilimia 59.3 ya mbegu za kiume kutoka kwa wanaume kutoka maeneo ya Marekani kaskazini, Ulaya, Australia na New Zealand yakishuka zaidi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: