Meneja Mauzo kampuni ya Mwananchi Communications Ltd, Aziz Msuya ameongoza timu ya waandishi wa habari wa kampuni hiyo kuuza nakala za gazeti la Mwanaspoti leo Alhamisi baada ya gazeti hilo kuwa na muonekano mpya katika mitaa mbalimbali ya Manispaa ya Morogoro.
Mwanaspoti ndilo gazeti la michezo linalopendwa zaidi na wasomaji kutokana na kusheheni habari mbalimbali za michezo ndani ya Tanzania, bara la Afrika na mabara mengine ya ulaya kutokana na kuwa na waandishi nguli waliobebea katika kuandika uchambuzi na makala kemkem.
0 comments:
Post a Comment