KIPA ALIYEDAKIA MCHEZO WA SIMBA SC DAY AFARIKI DUNIA RWANDA
Rwanda. Kipa wa Rayon Sports, Evariste Mutuyimana (Pichani) aliyedaka kwenye mechi dhidi ya Simba siku ya Simba Day jijini Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, amefariki dunia leo Jumanne kwenye Hospitali ya Kigali nchini Rwanda.
Shirikisho la Soka Rwanda (FERWAFA) limethibitisha kutokea kwa kifo cha mchezaji huyo, huku likitoa salamu za pole kwa klabu ya Rayon Sports.
Mchezaji huyo alijiunga na klabu hiyo msimu wa mwaka 2016/17 akitokea Sofapaka FC ya Kenya/mwanaspoti.co.tz
0 comments:
Post a Comment