BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MPALESTINA AWAPIGA RISASI NA KUWAUA WATU WATATU

Watu watatu raia wa Israel wameuawa kwa kupigwa risasi na raia wa Palestimna katika mlango wa kuingia kwenye makao ya walowezi wa kiyahudi eneo la Har Adara lililo ukingo wa magharibi.

Mtu mwenye bunduki wa umri wa miaka 37 kutoka kijiji kilicho karibu pia alipigwa risasi na kufariki baadaye.

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema mauaji hayo yamesababishwa na uchochezi upande wa palestina.

Mauaji hayo yanafanyika wakati mjumbe wa Rais Donald Trump eneo la Mashariki ya Kati Jason Greenblat, anapowasili Jerusalem kufufua mazungumzo kati ya Israeli na Palestina.

Ikulu ya Marekani inasema kuwa imejaribu kufanya mikakati wa kuyafufua mazungumzo tangu Donald Trump aingie madarakani mwezi Januari lakini hakujakuwa na dalili za kuwepo hatua.

Mazungumzo ya amani kati ya pade hizo mbili yalivunjika mwezi Aprili mwaka 2014.

Polisi wanasema kuwa mtu huyo mwenye silaha anayetajwa na vyombo vya habari nchini Israeli kama Nimer Jamal, alishambulia baada ya kugundua kuwa alishukiwa na walinzi karibu na mlango wa eneo la Har Adar.

Aliwapiga risasi walinzi wawili na polisi wa mpaka kwa karibu, na kumjeruhi vibaya mtu mwingine kabla ya kupigwa risasi na vikosi vya usalama.

Alitoka kijiji cha Beit Surik, karibu maili moja mashariki mwa Har Adar.

Eneo hilo liko karibu kilomita 18 kaskazini magharibi mwa Jurusalem.

Karibu Wapalestina 36,000 wana vibali vya kufanya kazi katika makao ya wayahudi ambapo ulinzi wa kuyalinda dhdi ya mashambulizi ni mkali.

Zaidi ya wayahudi 600,000 wanaishi karibu makao 140 yaliyojengwa tangu mwaka 1967, kwenye ukingo wa magharibi na Mashariki mwa Jerusalem.BBC
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: