BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MSHAMBULIAJI WA BARCELONA LIONEL MESSI AFICHA KIDONGE KATIKA SOKSI


Barcelona, Hispania. Lionel Messi ameonekana kitia mdomoni kitu alichokificha katika soksi kabla ya kuweka rekodi mpya katika mashindano ya Ligi ya Mabingwa.

Nyota huyo wa Barcelona alifunga bao lake la 100 katika mashindano yote ta Uefa akiiongoza klabu yake kushinda 3-1 dhidi ya Olympiakos kwenye Uwanja wa Nou Camp na alionekana ameficha siri ya mafanikio yake katika soksi.

Katika dakika ya 10, kwenye Uwanja wa Nou Camp, kamera za uwanjani zilimuonyesha Messi akichukua kidoge chake kutoka katika soksi na kukitia mdomoni.

Nyota huyo wa Argentina alitafuta kabla ya kwenda kuandika rekodi yake mpya.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Hispania, Messi alikuwa akitafuta kidonge cha glukozi ili kujiongezea nguvu.

Messi alifunga bao moja na kutegeneze lingine la Lucas Digne huku mchezaji wa Olympiakos, Dimitris Nikolaou akijifunga mwenyewe na kufanya kadi nyekundu aliyopewa Gerard Pique kukosa maana usiku huo. 


Kabla ya mapumziko Pique alikuwa ametolewa kwa kadi ya pili ya njano, wakati akijaribu kwenda kushambuliaji.Mwananchi
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: