BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WAFUGAJI SASA KUTOZWA FAINI YA SH300,000 ENDAPO MIFUGO ITAKANYAGA BARABARA YA LAMI


Mwanza. Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, imepitisha faini ya Sh300,000 kwa mfugaji atakayebainika kupitisha mifugo barabara kuu.

Akizungumza na kamati ya maendeleo ya kata za Lubili, Sumbugu na Isenegeja wilayani hapa juzi, mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Eliurd Mwaiteleke alisema faini hiyo itasaidia kupunguza uharibifu wa barabara unaofanywa na wafugaji.

“Barabara nyingi zimeharibika kwa sababu wafugaji wamekuwa wanapitisha mifugo yao, hivyo niwaagize viongozi wote wa vijiji na vitongoji kupitisha ushuru huo ili kukomesha vitendo hivyo,” alisema Mwaiteleke.

Baadhi ya wananchi wa kata hizo mbali ya kukubali agizo la mkurugenzi huyo, waliomba maofisa mifugo kuwaelekeza njia za asili zitakazotumika. Ofisa mifugo na uvuvi wa halmashauri hiyo, Chrispin Shami alisema kuna ng’ombe 160,996, mbuzi, 59,845 na kondoo 27,284 na kwamba watahakikisha wanapitisha agizo hilo kuwa sheria ili watakaokiuka wachukuliwe hatua.

Alisema wanajitahidi kufufua majosho ya ng’ombe ili kuwasaidia wafugaji kupeleka mifugo yao kupata chanjo.

Katika tukio jingine, mkuu wa wilaya ya Tarime mkoani Mara, Glorious Luoga amekutana na viongozi wa Kenya eneo la Maasai Mara kujadili mgogoro wa wizi na uporaji wa mifugo uliofanywa eneo hilo na kijiji cha Nyandage kata ya Nyanungu, wilayani Tarime.

Uporaji huo unadaiwa kufanyika wakati wananchi kutoka Kenya wakifuatilia mifugo iliyoibwa na nyayo kuonyesha kuingia nchini, wakiwa kijiji cha Nyandage walimpora mtoto ng’ombe wanne kama fidia ya walioibwa. Kiongozi wa ujumbe kutoka nchini Kenya, Anthony Mutuura alikemea kitendo hicho na kwamba, kinaweza kuzorotesha uhusiano mzuri baina ya nchi hizi mbili.

“Baada ya kuwahoji wakadai tunataka walete wetu nasi tuwape wao kwa sababu nyayo zimeishia kwao,” alisema .

Hata hivyo, Luoga aliwataka viongozi wa Maasai Mara kufika kijiji cha Nyandage kupewa ng’ombe wao walioonekana kijijini hapo.

Naye mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Nyandage, Kemahi Mirumbe alieleza kusikitishwa na uporaji ng’ombe uliofanywa akitaka utaratibu kufuatwa.

Ni takriban miaka 19 tangu wananchi wa nchi hizi mbili waache kuibiana mifugo, baada ya kukomeshwa na Serikali mwaka ya 1999.Mwananchi
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: