
JIJI LA KAMPALA.
Mwanasiasa wa upinzani nchini Uganda, juzi Alhamisi, amewataka wafuasi wake wa kiume kufanya mgomo wa kutoa unyumba kwa wake zao, mpaka pale wake zao hao, waahidi kutokipigia kura chama tawala katika uchaguzi ujao.
Uganda
Wachambuzi wengi wanaamini uchaguzi wa mwezi Februari utamrejesha tena madarakani Rais Yoweri Museveni na chama chake cha National Resistance Movement NRM. " Nyie mnasema ni wafuasi wa upinzani, wakati wake zenu wanakipigia kura chama cha NRM," amesema mwanasiasa huyo Stanley Kalembaye, akizungumza na kundi la watu katika mkutano ambao pia ulirushwa kupitia kituo cha televisheni cha NTV. "Mimi napendekeza muwanyime wake zenu haki ya ndoa ili wabadili vyama." amesema mwanasiasa huyo.
Kampala
Jiji la kampala
Shirika la habari la Reuters limesema mgombea huyo wa chama cha MDC ambaye anawania umeya wa jiji la Mbarara, amesema wanaume hawana budi kuwaelewesha wake zao.
"wakishindwa kuelewa kwa njia ya mazungumzo, basi wawanyime unyumba." amesema mgombea huyo.
Migomo ya kunyima unyumba imekuwa silaha inayotumika sehemu kadhaa barani Afrika, lakini mara nyingi huwa ni wanawake dhidi ya wanaume.
Maelfu ya wanawake wa Kenya mwaka jana walidai kuwanyima haki hiyo wanaume zao ili kushinikiza kumalizika kwa ghasia baada ya uchaguzi, huku wanawake wa Liberia pia wakifanya hivyo katika kampeni inayosemwa kusaidia kwa kiasi kikubwa kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa muda mrefu.
Nafikiria -- Kama NRM nao wakiamua kutumia mbinu hiyo, sijui itakuwaje.....
0 comments:
Post a Comment