
Bwana mmoja nchini Marekani ambaye huamka na kutembea akiwa usingizini, amejiamsha kwa mtindo wa aina yake. Bwana huyo Sandford Rothman wa Boulder huko Colorado, alisikia mlio mkubwa,wakati akiwa ndotoni, na aliposhituka akakuta amejipiga risasi kwenye goti lake.
Bunduki
Milimita 9
Kwa mujibu wa polisi wa huko, Bwana Rothman, mwenye umri wa miaka sitini na mitatu, huweka bastola yake ndogo yenye milimita 9, karibu na kitanda chake. Gazeti la Telegraph limesema hakuna ulevi au dawa zozote za hospitali zimehusishwa na tukio hilo.
Bwana huyo alitibiwa majeraha yake katika hospitali ya jamii ya Boulder kabla ya kuruhusiwa kwenda nyumbani.
Pistol
'Mguu wa kuku'
Tukio hili limekuja, siku chache baada ya bwana mwingine Darrel Elam pia wa Marekani kujipiga risasi, baada ya kuweka bastola yake kwenye mfuko wa nyuma wa suruali. Darrel alifyatua kwa bahati mbaya bastola hiyo, ambapo risasi ilipita kwenye kalio lake la kushoto, na kuteremka kupitia mguu hadi kwenye goti.
Waswahili wanasema, mtoto akililia wembe, mpe, inawezekana kabisa, jamaa hawa hawakupewa wembe walivyokuwa wadogo.
0 comments:
Post a Comment