Wanamgambo wa kundi la al-Shabab la nchini Somalia.
WATU wenye silaha wamemuuwa mwandishi
wa habari maarufu wa Somalia eneo ambalo limekuwa hatari kwa watu wenye
taaluma hiyo duniani.
Katika tukio hili watu wasiojulikana jana walimuuwa kwa kumfyatulia risasi, Yusuf Ali Osman anayejulikana sana kwa jina la farey katika wilaya ya dharkenely mjini Mogadishu .
Osman mkurugenzi wa zamani wa radio Mogadishu alikuwa anafanya kazi katika wizara ya habari ya Somalia.
Jumuiya ya waandishi wa habari wa somalia iliyoko uhamishoni nchini Kenya katika taarifa yake ili sema kuwa Osman ni mwandishi wa habari wa nane kuuwawa nchini somalia katika kipindi cha mwaka 2012.
Katika tukio hili watu wasiojulikana jana walimuuwa kwa kumfyatulia risasi, Yusuf Ali Osman anayejulikana sana kwa jina la farey katika wilaya ya dharkenely mjini Mogadishu .
Osman mkurugenzi wa zamani wa radio Mogadishu alikuwa anafanya kazi katika wizara ya habari ya Somalia.
Jumuiya ya waandishi wa habari wa somalia iliyoko uhamishoni nchini Kenya katika taarifa yake ili sema kuwa Osman ni mwandishi wa habari wa nane kuuwawa nchini somalia katika kipindi cha mwaka 2012.
katika taarifa hiyo jumuiya hiyo ilisema kuwa inaumiza na
kuvunja moyo hasa kwa kuwapoteza mwandishi wa habari mahiri kila mwezi.
Mwakilishi maalumu wa umoja wa mataifa kwa ajili ya Somalia Augustine Mahiga alilaani kuuwawa kwa Osman na kutoa mwito tena kwa maafisa wa Somalia kufanya uchunguzi wa mashambulizi kwa waandishi wa habari.
Mwakilishi maalumu wa umoja wa mataifa kwa ajili ya Somalia Augustine Mahiga alilaani kuuwawa kwa Osman na kutoa mwito tena kwa maafisa wa Somalia kufanya uchunguzi wa mashambulizi kwa waandishi wa habari.
0 comments:
Post a Comment