BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAANDALIZI YA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA YA KUHITIMU ELIMU YA MSINGI NCHINI KUANZA KESHO.

Wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Bungo Manispaa ya Morogoro wakifanya usafi kwa kufuta  katika madawati katika moja ya darasa ya shule hiyo kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mitihani ya taifa ya kuhitimu elimu ya msingi inayoanza kesho nchini kote.
 Sehemu ya wanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi Bungo Manispaa ya Morogoro wakiweka namba katika madawati ikiwa maandalizi ya mitihani ya taifa ya kuhitimu elimu.

Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Bungo Manispaa ya Morogoro, Roman Luwoga akihakiki fomu za maombi ya wanafunzi wa darasa la saba (TS9) kwa ajili ya maandalizi ya kujiunga na masomo ya elimu ya sekondari mara baada ya kuhitimu elimu ya  darasa la saba ambapo kesho wanafunzi wa darasa la saba wanafanya mitihani ya kuhitimu elimu hiyo nchini kote.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: