BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WAKUU WATATU WAANDAMIZI WA JESHI LA POLISI WASIMAMISHWA KAZI KENYA.


Mkuu wa polisi mkoani Rift Valley John M'mbijiwe anayedaiwa kuwa na uhusiano na mtu huyo mlaghai,John Waiganjo ingawa alikana kumfahamu.

MAAFISA watatu waandamizi wa polisi nchini Kenya, wamesimamishwa kazi kuhusiana na sakata ya mtu mmoja ambaye aliwalaghai watu kuwa yeye ni naibu kamishna mkuu wa polisi kwa zaidi ya miaka mitano.
Mkuu wa polisi mkoani Rift Valley John M'mbijiwe anayedaiwa kuwa na uhusiano na mtu huyo mlaghai,John Waiganjo ingawa alikana kumfahamu ni mmoja wa wale waliofutwa kazi.
Mwenyekiti wa tume ya kuwaajiri maafisa wa polisi KPSC Johnstone Kavulundi, amesema maafisa hao watatu wametajwa kuhusika kwa njia moja au nyingine na kashfa hiyo.
Wiki iliyopita, Joshua Waiganjo, alifikishwa mahakamani, kwa kujifanya afisa mwandamizi wa polisi katika mkoa wa Rift Valley.
Mshukiwa huyo amekanusha madai hayo.
Ripoti zinasema kuwa ulaghai huo ulifichuliwa, wakati aliposafiri kwa ndege ya polisi, kwenda kuchunguza mauaji wa maafisa 42 wa polisi waliouawa na wezi wa ng'ombe katika bonde la Suguta, tukio ambalo ndilo mbaya zaidi kuwahi kutokea katika historia ya taifa hilo.
Rais Mwai Kibaki ameagiza uchunguzi kamili kuhusiana na tukio hilo.
Kavulundi amesema kuwa mkuu wa polisi mkoani humo John M'Mbijiwe, afisa mkuu wa kitengo cha polisi cha kupambana na wezi wa mifugo ASTU Remi Ngugi na afisa mkuu wa polisi wilayani Njoro Peter Nthiga wamesimamishwa kazi.
Amesema watatu hao huenda wakahujumu uchunguzi ikiwa wataendelea kusalia madarakani.
Joshua Waiganjo amesemekana kuwafuta kazi na kuwaajiri maafisa wengine wa polisi katika mkoa wa Rift Valley wakati huo.
Baada ya kukana mashtaka hayo, kesi hiyo ilihairishwa ili kumruhusu mshukiwa huyo kutafuta matibabu kutokana na ugonjwa wa kisukari katika hospitali moja nchini humo. 

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: