BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI SHABAANI KIMEA AFARIKI DUNIA JIJINI DAR ES SALAAM.


 
KAMISHNA Msaidizi wa Polisi (ACP) Shabani Kimea (54) amefariki dunia machi 27 mwaka huu katika Hospitali ya Hindu Mandal jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa kwa ajili ya matibabu ya maradhi.

Taarifa iliyotolewa na kuthibitishwa na  Msemaji wa Polisi Advera Senso, imesema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Familia ya Marehemu tayari imefanikisha kuusafirisha mwili wa marehemu kwenda Kijijini kwao Mwera mkoani Tanga, kwa ajili ya Mazishi.


Senso alisema Kufuatia msiba huo Jeshi la Polisi nchini limepata pengo kubwa kwa kuondokewa na kamishina huyo kwa kuwa alikuwa mtendaji hodari hali iliyopelekea kutunukiwa nishani ya utumishi wa muda mrefu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Jakaya Mrisho Kikwete.

Alisema Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema amezipokea taarifa za kifo hicho kwa huzuni hasa ukizingatia hivi sasa Askari mmoja anahudumia watu takribani 1300 hadi 1500 hivyo kufariki kwa Ofisa, Mkaguzi au Askari mmoja ni pengo kubwa kwa Jeshi la Polisi na Watanzania hasa katika nyanja ya usalama na ameitumia familia ya marehemu salamu za rambirambi.

ACP Kimea alijiunga na Jeshi la Polisi Mwaka 1985 na kupandishwa vyeo mbalimbali hadi kufikia Cheo cha Kamishna Msaidizi wa Polisi ambapo mpaka mauti yanamkuta alikuwa mkuu wa Kitengo cha Mipango ya Raslimaliwatu (Human Resource and Planning) Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na nafasi nyingine alizowahi kushika ni pamoja na kuwa Mkuu wa Upelelezi wilayani Misungwi, Mkuu wa Polisi wilayani Misungwi na Geita pamoja na Mnadhimu Mkuu wa Polisi Mkoani Morogoro.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: