TAASISI ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislam Tanzania, imepongeza uamuzi
wa Mufti Shaaban Bin Simba wa kuwakutanisha viongozi wa dini ya Kiislamu
na Kikristo, ili kutafuta amani ya nchi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, jana Katibu
Mkuu wa taasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania, Sheikh
Khamis Mataka alisema hatua hiyo ya kuwakutanisha viongozi hao,
itasaidia kulinda amani ya nchi kwa njia ya mazungumzo.
Sheikh
Mataka, alisema hatua hiyo ya Mufti ni muhimu ambayo alianza kuinyoosha
kupitia mkutano wa mano na uvumilivu ulioandaliwa na taasisi hiyo
Februari 20, mwaka huu.
“Taasisi ya Masheikh na Wanazuoni wa
Kiislamu, tunawaomba viongozi wa dini ya Kikristo watoe ushirikiano
katika kufanikisha dhamira njema ya Mufti na kwamba bila ushirikiano wao
ni vigumu kuirejesha afya ya jamii inayozorota kila uchao katika hali
njema,” alisema Sheikh Mataka.
Akizungumzia ziara ya Katibu Mkuu
wa Shirikisho la Ulimwengu wa Kiislamu (RABITA), Dk. Abdullah Al-Turki,
alisema kuwa zimekuwa na mafanikio makubwa kwa nchi.
MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment