BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIS MSTAAFU AWAMU YA TATU BENJAMIN MKAPA: TUSITANGULIZE UDINI KWENYE KATIBA.

Kwa ufupi
Ujumbe wa amani na tahadhari ya umakini kwenye utoaji maoni kwenye Katiba ndiyo vilitawala wakati wa misa za Sikukuu ya Pasaka zilizofanyika sehemu mbalimbali nchini jana na juzi. 
 http://www.mwananchi.co.tz.
DAR ES SALAAM
UJUMBE wa amani na tahadhari ya umakini kwenye utoaji maoni kwenye Katiba ndiyo vilitawala wakati wa misa za Sikukuu ya Pasaka zilizofanyika sehemu mbalimbali nchini jana na juzi.

Miongoni mwa waliotoa hotuba wakati wa sikukuu hiyo ni pamoja na Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, ambaye alikuwa mkoani Mtwara; na Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo aliyekuwa jijini Dar es Salaam.
Mkapa akataa udini.
Rais mstaafu Mkapa alitumia fursa ya kutoa salamu katika Kanisa Katoliki mjini Masasi kuliasa taifa kujiepusha na utoaji wa maoni ya Katiba kwa misingi ya dini.
Mkapa alisema katiba ijayo haipaswi kuwa na itikadi za kidini kwa kuwa zinaweza kuliangamiza taifa.
“Wapo watakaopata uwakilishi kupitia rasimu ya Katiba ya nchi. Namwomba Mwenyezi Mungu awape mwanga, muhakikishe jambo moja tu ambalo litakuwa msingi mkubwa wa amani na maendeleo na umoja wa taifa letu.
Watupatie Katiba ambayo inatoa fursa kamilifu ya kila mtu kuwa na imani yake.
“Katiba inayoheshimu imani ya kikatiba na imani zote zinazofanywa na wananchi wa Kitanzania…Vilevile ihakikishe kwamba dola au nchi yetu haina imani rasmi kama vile nchi yetu isivyo ya kabila moja, hivyo haiwezekani kuwa na Katiba ambayo inatambua kwa dhana au maandalizi ya vipengele mbalimbali kwamba kuna udini, haiwezekani.”
Askofu na Muungano.
Watanzania wametakiwa kuwapuuza watu wanaohubiri kuuvunja Muungano kwani watu hao wana agenda binafsi ambazo si kwa faida au masilahi ya nchi, bali wao na baadhi ya mataifa yanawafanya vibaraka wa kuvuruga amani na utulivu uliodumu kwa miaka mingi.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mhashamu Askofu Gervas Nyaisonga wa Jimbo Katoliki la Dodoma wakati wa misa ya Pasaka ambayo iliyofanyika kitaifa katika Kanisa Kuu la Kiaskofu la Mt. Paulo wa Msalaba mjini humo.
Askofu Nyaisonga alisema hata kama kuna baadhi ya matatizo katika Muungano, yanapaswa kuboreshwa badala ya kuuvunja kabisa Muungano ambao kimantiki umeijengea nchi heshima.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: