BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

YANGA SC WALIVYOIUA OLJORO LIGI KUU YA VODACOM NA KUIVUA UBINGWA SIMBA UWANJA WA TAIFA DAR ES SALAAM.

Mshambuliaji wa Yanga SC, Didier Kavumbangu akiwatoka mabeki wa JKT Oljoro katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga ilishinda 3-0.
Kiungo wa Yanga, Haruna Niyonzima (kushoto) akimtoka kiungo wa JKT Oljoro, mbele ya refa Amon Paul
Didier Kavumbangu akigombea mpira na beki wa JKT Oljoro
Hamisi Kiiza wa Yanga katikati akimtoka beki wa Oljoro kulia. Kushoto ni mshika kibendera namba moja, John Kanyenye akifuatilia mwenendo
Frank Domayo kulia akipenyeza mpira pembeni ya kiungo wa Oljoro, Hamis Saleh
Didier Kavumbangu akigombea mpira na beki wa Oljoro
Didier Kavumbangu akiwania mpira wa juu dhidi ya beki wa JKT Oljoro nyuma yake.
Didier Kavumbangu akiwa amemuangukia kipa wa JKT Oljoro, Mussa Lucheke huku beki Nurdin Mohamed akiondoka na mpira

Sekeseke; Beki wa Oljoro akiwa hewani kupiga mpira wa kichwa wakati wa kizazaa langoni mwao

Hamisi Kiiza akikosa bao baada ya kipa Mussa Lucheke kuokoa mpira ambao hata hivyo ulimponyoka...

Hamisi Kiiza akijaribu kumpokonya mpira kipa wa Oljoro, Mussa Lucheke
Kipa wa JKT Oljoro, Mussa Lucheke akijaribu kupangua mpira wa juu bila mafanikio. Mpira ulimpita ukaokolewa na beki ukamkuta Nadir Haroub 'Cannavaro' akaukwamisha nyavuni kuipatia Yanga bao la kwanza.
Kikosi cha Yanga.
Kikosi cha JKT Oljoro.
Simon Msuva akifumua shuti kufunga bao la pili la Yanga.
Kiungo Athumani Iddi 'Chuji' akiwa ameruka na kipa wa JKT Oljoro, Mussa Lucheke.
Wachezaji wa Yanga Nadir Cannavaro, Haruna Niyonzima na Athumani Iddi wakimlalamikia refa Amon Paul kushoto
Said Bahanuzi wa Yanga akifumua shuti pembeni ya Hamisi Kiiza na beki wa JKT Oljoro, Salim Mbonde, Bahanuzi alifunga, lakini refa akasema alikuwa ameotea kabla ya kupiga mpira.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: