BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

DUH KUMBE !!!!..DIDIER GROGBA ANA ROHO MBAYA.

Didier Drogba dreht für Galatasaray Istanbul ein bereits verloren geglaubtes Spiel. (Quelle: imago/Contrast)
MSHAMBULIAJI Didier Drogba ameendelea kuwa mwiba kwa Arsenal akikumbushia enzi zake alipokuwa na jezi ya Chelsea, baada ya mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 35 leo kufunga mabao mawili na kuiwezesha klabu yake, Galatasaray kutwaa Kombe la Emirates.Disappointment: Arsenal manager Arsene Wenger looks on during his side's defeat
Kweli, ni mashindano ya kirafiki na hayana maana yoyote katika msimu, lakini lilikuwa kama pigo lingine kwa kikosi cha Arsene Wenger.
 
Mfaransa huyo aliwaka ile mbaya kana kwamba mashindano hayo yana maana yoyote. Alimfokea refa wa akiba, Andre Marriner baada ya refa Jon Moss kuwazawadia penalti wapinzani dakika 12 kabla ya filimbi ya mwisho kutokana na Ignasi’s Miquel kumsukuma mshambuliaji huyo wa Ivory Coast.

Drogba alikwenda mwenyewe kupiga penalti hiyo na kumpeleka upande tofauti kipa Wojciech Szczesny na mpira alipoupiga. 
Drogba akafunga tena zikiwa zimesalia dakika nne, baada ya kupokea pasi ya Wesley Sneijder na kumuacha Per Mertesacker, kabla ya kumtungua tena Szczesny.
 
Arsenal ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao katika mchezo huo dakika ya 38, mfungaji Theo Walcott. 
 
Katika mchezo huo, kikosi cha Arsenal kilikuwa; Szczesny, Jenkinson, Sagna, Mertesacker, Gibbs/Miquel dk69, Arteta, Ramsey, Oxlade-Chamberlain, Cazorla/Zelalem dk61, Walcott na Sanogo/Giroud dk61.
 
Galatasaray Muslera; Semih, Riera, Chedjou, Eboue, Melo/Sarioglu dk66, Engin Baytar/Gulselam dk32,Altintop/Colak, dk45, Amrabat, Elmander/Drogba dk45, Umut Bulut/Sneijder dk45.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: