BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MKUU WA MKOA APIGA STOP MKUTANO WA HARADHA WA NAPE NNAUYE MTWARA.

Nape NnauyeNAPE NNAUYE.

Na Florence Sanawa, Mtwara.
OFISI ya Mkuu wa Mkoa wa Mtwara imekunjua kucha na kutangaza kutofanyika kwa mkutano wa hadhara wa Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye. 


Hatua hiyo imekuja baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kuzuia mikutano ya hadhara kutokana na vurugu zilizotokea mkoani humo kupinga ujenzi wa bomba la gesi. 

Akizungumza na wana CCM mkoani hapa baada ya kupokea barua ya kuzuiwa kufungua matawi na mkutano wa hadhara, Nape alisema sasa umefika wakati kwa Serikali kuangalia sheria na zuio hilo na kwa kina.
Alisema sheria hiyo pamoja na kutungwa na Serikali ya CCM, lakini bado haiendi na wakati, ikiwemo kuwazuia viongozi kuwafikia wananchi na kusikiliza kero zao. 

“Ni kweli ilikuwa twende kuzindua mashina kwenye maeneo yenu, lakini liko agizo la Serikali ya CCM, kupitia kwenu hatuoni haja ya kuendelea na sheria hii, iko haja ya kufungua mikutano iruhusiwe ili demokrasia zizidi kumea. 

“Kwa mtazamo wangu sheria hii inabaka demokrasia, lazima demokrasia isibakwe hata kidogo, kama hali ni mbaya ni wajibu kwa Serikali kulinda raia na mali zao na hiyo ndiyo kazi yao, badala ya kuwazuia watu kufanya shughuli za kisiasa,” alisema Nape. 

Katibu huyo wa NEC, Itikadi na Uenezi, alisema CCM ndiyo yenye Serikali ambapo aliahidi kwenda kushauriana na viongozi ili kuona namna ya kuondoa zuio hilo. 

“Nakwenda kushauriana na serikali na sioni namna ambayo masikio yatavuka kichwa, tutakubaliana shughuli za kisiasa zitafunguliwa na mambo yaende vizuri,” alisema. 

Kutokana na hali hiyo, Nape alilazimika kuzungumza na viongozi wa chama hicho katika ukumbi wa mikutano wa CCM Wilaya ya Mtwara, ambako aliwataka kuhakikisha wanasimamia uhai wa chama katika maeneo yao sambamba na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2010. 

Katika kikao hicho cha ndani, Nape alikabidhi bendera kwa viongozi wa mashina, pikipiki tatu kwa vikundi vya Pentekoste na Jionee zilizotolewa na Mbunge wa Mtwara Mjini, Hasnen Murji (CCM).MTANZANIA
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: