BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

RAIS WA CHUO BADO HARUDISHA KUMBUKUMBU ZAKE ZA AKILI.

Mwanza.
Rais wa Serikali ya Wanafunzi Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Tiba cha Bugando (Cuhas), Musa Mdede ambaye alitoweka katika mazingira ya kutatanisha Juni 17, mwaka huu bado hatambui alikuwa wapi.
Kiongozi huyo wa wanafunzi ambaye aliokotwa na wasamaria, amewekwa kwenye ulinzi maalumu na familia yake.
Makamu wa Rais Cuhas, Atukuzwe Mordecai alisema bado Mdede hatambui alikokuwa licha ya kukumbuka kwamba siku moja kabla ya kupotea alikwenda Dar es Salaam kwenye kikao cha Umoja wa Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (Tahliso).
Mordecai alisema kutokana na hilo, walishauriwa kumweka kwenye uangalizi maalumu kwa kushirikiana na familia yake na kwamba hakuna mtu anayeruhusiwa kwenda kumwona.
“Mdede kwa sasa yupo kwenye uangalizi hadi hapo atakapokuwa na kumbukumbu,” alisema Mordecai na kuongeza:
“Kuna watu wengi wanataka kumwona na kuzungumza naye, lakini kwa jinsi alivyo sasa hawezi kuzungumza kitu chochote hadi hapo atakapokuwa na kumbukumbu vizuri, kwani kwa sasa hatambui kitu gani kilitokea.”
Mmoja wa ndugu zake, Chenga Gudluck alisema kwa sasa hali yake inaendelea vyema licha ya kukosa kumbukumbu.
“Kiafya yupo vyema, lakini mpaka sasa bado hana kumbukumbu alikuwa wapi. Kiusalama tumeshauriwa akae sehemu maalumu ambayo atakuwa yeye tu na watu wake wa karibu,” alisema.
Akizungumza kwa simu jana, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Ephren Malley alisema uongozi wa chuo hauna cha kusema hadi polisi watakapomaliza uchunguzi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Valentino Mlowola alisema bado wanaendelea na uchunguzi ili kubaini alipotea katika  mazingira gani.MWANANCHI
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: