BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAMILIONI YA MAHUJAJI WA DINI YA KIISLAMU WASIMAMA KATIKA MLIMA ARAFA WAKIOMBA DUA NCHINI SAUDI ARABIA,

20120509-Arafat ilgrims_cover roads _plains_and_mountain.jpg
Mahujaji zaidi ya milioni mbili wa Nyumba Tukufu ya Mwenyezi Mungu jana wamesimama katika uwanja wa Arafa kutekeleza nguzo kuu ya ibada ya Hija ambako wameshinda wakiomba dua na kumtaradhia Mola Muumba.

Wageni hao wa Nyumba ya Mwenyezi Mungu walishinda katika uwanja huo na wamenza kuondoka hapo baada ya kuzama jua wakielekea Muzdalifa.

Ripoti zinasema kuwa hadi jioni ya jana hakukuripotiwa tukio lolote la kutia wasiwasi.


Mahujai hao watakesha Muzdalifa na kumdakia Mina katika siku ya kumi ya Dhulhaji kwa ajili ya ibada ya kumpiga mawe shetani na kuchinja mnyanya wa sadaka.


Serikali ya Saudi Arabia inasema kuwa karibu Waislamu milioni moja na nusu kutoka nje ya nchi wanatekeleza ibada ya Hija mwaka huu mbali ya mamia ya maelfu ya Mahujaji kutoka maeneo mbalimbali ya Saudia kwenyewe.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: