BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WATU SABA WAFARIKI DUNIA NA 15 WAKINUSURIKA BAADA YA KUPIGWA NA RADI WAKATI WAKIWA KATIKA MAOMBI MLIMANI.


Nyumba walimokuwa wanafanyia mambo watu wa Wawi iliteketea yote
Watu saba wa jamii moja nchini Colombia wamefariki baada ya kupigwa na radi wakiwa katika shughuli ya maombi katika eneo moja milimani Kaskazini mwa nchi hiyo.

Viongozi kutoka kabila la Wiwa walikuwa wanafanya maombi walipopigwa na radi.

Watu wengine 15 walijeruhiwa.
Walionusurika waliokolewa na jeshi na kupelekwa hospitalini mjini Santa Marta.

Wengi wa walioathiriwa wanapokea matibabu baada ya kupata majeraha mabaya.

'madhabahu yateketea'

Mkasa huo ulitokea Jumapili usiku karibu na mji wa Guachaca, katika milima ya Sierra Nevada.

Takriban watu 60 walikuwa wamekusanyika kwa sherehe maalum ya maombi, ndani ya nyumba ndogo ya nyasi wakati ilipopigwa na radi.

Nyumba hiyo iliteketea yote.

''Tunawaombea watu wa jamii ya Sierra Nevada,'' alisema Rais Juan Manuel Santos kwenye akauti yake ya Tiwtter.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: