BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WALIOMBAKA MSICHANA GESTI KISHA KUMWINGILIA KINYUME NA MAUMBILE NA KUSAMBAZA PICHA ZA NGONO ZA VIDEO WAFIKISHWA KWA KILATO MOROGORO

Mmoja wa ndugu wa watuhumiwa wa usambazaji wa picha za video za utupu za mmoja wa wasichana akiangua kilio wakati gari lililowabeba watuhumiwa hao likiondoka mahakama ya hakimu mkazi Morogoro,


VIJANA wawili, Zuberi Thabiti (30) mkazi wa Mbarali, mkoani Mbeya na Iddy Adamu (32) mkazi wa Makambako wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Morogoro kwa tuhumaza za kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 21 katika tukio linalodaiwa kufanyika Aprili 27 mwaka huu Dakawa mkoani hapa.

Katika mashtaka wanayokabiliana nayo ni pamoja na kumbaka msichana huyo, kumpiga picha za utupu za video na kuzisambaza katika mitandao ya kijamii, katika nyumba ya kulala wageni ya Titii iliyopo Dakawa wilayani Mvomero.

Watuhumiwa hao wamefikishwa mahakamani leo na wengi wanne kati ya 11 wakiwemo waliopokea picha hizi za video na kusambaza video.
Kushoto ni Zuberi Thabiti (30) mkazi wa Mbarali mkoani Mbeya na Iddy Adamu (32) mkazi wa Makambako 

Wengine wanaotuhumiwa kusambaza picha hizo za utupu za video ni pamoja na Rajabu Salehe (26), Saidi Athmani (26), Musini Ngai (36) Saidi Mohamedi (24), John Peter (24), Hassan Ramadhan (27), Ramadhan Ally (27), Musini Ngahyi na Ramadhan Ngonja.

Watuhumiwa walinyimwa dhamana na kupelekwa mahabusu ya magereza ya mkoa kwa kile kilichoelezwa na waendesha mashtaka wa serikali kuwa watavuruga ushahidi ambapo watuhumiwa hao watafikishwa tena Juni Mosi mwaka huu.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: