BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

HUZUNI, HOFU ZATAWALA PENDEKEZO LA KUFUTWA KWA KIJIJI CHA NGAITE KILOSA MORO



Juma Mtanda, Morogoro-jphtjuma@gmail.com
Kaya zaidi ya 300 zenye wakazi 1767 katika kijiji cha Ngaite kata ya Parakuyo wamekumbwa na wasiwasi na hofu baada ya diwani wa kata hiyo, Ibrahim Oloishuro Kalaita kuitisha mkutano wa kijiji na kuwasilisha pendekezo la kufutwa kwa kijiji hicho kutokana na sababu mbalimbali wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro.

Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika shule ya msingi Ngaite jana, Oloishuro Kalaita alisema kuwa halmashauri ya wilaya ya Kilosa kupitia idara ya ardhi na maliasili imetoa pendekezo la kufutwa kwa kijiji hicho jambo lililopelekea wananchi hao kukumbwa na mshtuko na wasiwasi wa namna ya kuanza maisha mapya.

“Niliagiza viongozi wa kijiji waitishe mkutano mkuu wa kijiji kisha waeleze sababu za pendekezo la kufutwa kwa kijiji la Ngaite lililopendekezwa na halmashauri ya wilaya ya Kilosa kupitia idara ya ardhi na maliasili lakini mapokeo yamekuwa tofauti na kuzua hofu na wasiwasi mkubwa juu ya maisha yao.”alisema Oloishuro Kalaita.

Jana (Juzi) nilifanya mkutano wa kijiji wa ufafanuazi juu ya pendekezo hilo lakini mwitikio wa wananchi hao juu ya jambo hilo bado umeendelea kukubikwa na hofu.

wakizungumza katika mkutano huo, Christina Kiamba (49) na Elizaberth Changalima (61) walisema kuwa wamestushwa na taarifa ya pendekezo la kufutwa kwa kijiji cha Ngaite kutokana na uwepo wa kuimarika kwa huduma za jamii ikiwemo shule.

“Ngaite tayari imekuwa na maendeleo na ina jamii kubwa sasa kama kijiji kitafutwa jamii hii yenye kila aina ya rika serikali itaipeleka wapi ?...tumeambiwa na viongozi wetu mipango iliyopo ni kuimarisha miundombinu ya barabara na ujenzi wa jengo la zahanati.”alisema Chritina.

Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa, Kessy Mkambala akitoa ufafanuzi juu ya pendekezo la halmashauri yake kupitia idara ya ardhi na maliasili kufutwa kwa kijiji cha Ngaite alisema kuwa wananchi wa kijiji hicho wasipatwe na hofu.

Mkambala alisema kuwa kijiji cha Ngaite hakitafutwa na wananchi wataendelea kuishi eneo hilo isipokuwa mamlaka ya kijiji hicho ndio yatafutwa na mamlaka yatakuwa katika kijiji mama cha Malangali kata ya tarafa.

“Halmashauri imetoa mapendekezo kupitia watalaamu la kufutwa kwa mamlaka ya kijiji cha Ngaite na mapendekezo hayo yatapishwa na baraza la madiwani kama wataridhia pendekezo hilo ama kukataa.”alisema Mkambala.

Mkambala alisema kuwa moja ya sababu za pendekozo la kufutiwa kwa mamlaka ya kijiji cha Ngaite ni pamoja na mchakato wa kuanzisha kijiji cha Ngaite haukuzingatia taratibu zote za kisheria ya serikali za mitaa namba 7 ya 1982 (sura ya 289/2002).

Sheria ya ardhi namba 5 1999 inazitaka vijiji kuwa na kaya zisizopungu 250 nna kuwa na eneo ambalo mipaka yake inatambulika.alisema Mkambala.
Aliongeza sababu nyingine kuwa ni kijiji kuwa na eneo la kutosha la shughuli za kiuchumi na jamii za sasa na za baadaye pamoja na njia za mawasiliano hususani barabarani.

“Kijiji chote cha Ngaite kipo ndani ya shamba la mifugo la Narco lenye hatimiliki hivyo kusababisha kijiji kutokuwa na ardhi hata kijiji hicho kinaanzishwa kamati ya maendeleo ya kata husika hakuidhinishwa na kata husika maombi ya kuwa kijiji.”alisema Mkambala.

Kijiji cha Ngaite ni miongoni mwa vijiji vitatu vinavyounda kata ya Parakuyo, kijiji hicho kilianzishwa Agosti 22 mwaka 2014 kwa mujibu wa tangazo la serikali namba 301.CHANZO/MTANDA BLOG
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: