BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAGOLI 10,876 YAFUNGWA NA WAFUNGAJI 22 LIGI DARAJA LA KWANZA NETIBOLI TZ BARA MORO

Kiungo msambazaji mipira ya timu ya netiboli ya Uhamiaji, Betina Kazinja akitafuta mbinu ya kutoa pasi kwa mwenzake wakati wa mashindano ya netiboli ligi daraja la kwanza Tanzania bara katika mchezo wa mwisho dhidi ya Polisi Morogoro ambapo katika mchezo huo Uhamiaji ilishinda kwa magoli 44-40 na kutwaa ubingwa wa ligi hiyo uwanja wa jamhuri Morogoro.


Juma Mtanda, jphtjuma@gmail.com

Jumla ya magoli 10,876 yamefungwa na washambuliaji 22 katika mashindano ya netiboli ligi daraja la kwanza Tanzania bara 2016/2017 katika michezo 40.

Idadi hiyi inatokana magoli yaliyoamua ushindi yakiwa 5393 huku walinzi wa timu 11 wakiruhusu kufungwa  jumla ya magoli 5483 katika michezo hiyo 40.


Timu ya netiboli ya Uhamiaji iliibuka na ubingwa bila kupoteza mchezo wowote baada ya kushinda michezo yote 10 na kukusanya pointi 20 ikiwa imefunga magoli 779 na kufungwa magoli 237 katika ligi hiyo iliyohusisha jumla ya michezo 40 na kumalizika hivi karibu katika uwanja wa jamhuri mkoani Morogoro.     


Akizungumza na gazeti hili mjini hapa, Mwenyekiti wa Chaneta Tanzania, Anna Kibira alisema kuwa mashindano hayo yalishirikisha jumla ya timu 11 ikiwa na washambuliaji 22 ambao wamefunga magoli 5393 wakati walinzi wa kila timu nao wakiruhusu kufungwa jumla magoli 5483 katika michezo hiyo.


Kibira alisema kuwa ligi ya mwaka huu ilikuwa na ushindani mkubwa hasa baada ya timu ya netiboli ya Polisi Morogoro kufanya usajili wa nguvu uliopelekea Uhamiaji kushinda kombe la ligi hiyo kwa mbinde katika mchezo wao wa mwisho uliohesabiwa kama fainali kutokana na timu hizo kulingana pointi 18 katika michezo tisa kabla ya kukutana katika mchezo wa mwisho na Uhamiaji kushinda.


“Ligi daraja la kwanza mwaka huu ilikuwa na ushindani mkubwa na hii imetokana na usajili uliofanywa na timu shiriki lakini Polisi Morogoro niwapongeze kwa kufanya usajili wa nguvu na kuleta changamoto kubwa kwa Jeshi Stars na Uhamiaji.”alisema Kibira.


Akitaja msimamo wa ligi hiyo, Kibira alisema kuwa Uhamiaji ndio mabingwa wa msimu wa mwaka 2016/2017 ikitetea ubingwa huo kwa mara ya pili mfululizo huku Polisi Morogoro ikishika nafasi ya pili kwa kukusanya pointi 18 baada ya kushinda michezo tisa na kupoteza mmoja ikiwa imefunga magoli 659 na kufungwa 325.


Nafasi ya tatu imeshikwa na Jeshi Stars yenye pointi 14 ikifunga magoli 650 ikifungwa magoli 359 na kupoteza michezo mitatu huku Madini Arusha iliyopoteza michezo mitatu kutoa sare mchezo mmoja imeshika nafasi ya nne na pointi 13 ikifungwa magoli 401 na kufunga magoli 531 wakati Tumbaku Morgoro imefunga magoli 606, kufungwa magoli 457 na kupoteza michezo minne baada ya kukusanya pointi12 ikiwa nafasi ya tano.


Polisi Arusha iliyopoteza michezo mitano imeshika nafasi ya sita kwa kuwa na pointi 10 baada ya kufungwa magoli 523 na kufunga magoli 512 huku Jiji Arusha yenye pointi tisa nafasi ya saba imefunga magoli 465 na kufungwa magoli 470 na sare mchezo mmoja.


Michezo mingine timu ya Kikosi cha kutengeza sare za jeshi (CMTU) imeshika nafasi ya nane baada ya kupoteza michezo sita ikikusanya pointi nane ikifunga magoli 447 na kufungwa magoli 452, Jiji Tanga imemaliza nafasi ya tisa na pointi nne baada ya kushinda michezo miwili kufungwa michezo nane kwa kufunga magoli 291 na kufungwa 646.


Ras Kagera iliyoshinda mchezo mmoja imemaliza ikiwa na pointi mbili ikipoteza michezo tisaa ikifungwa magoli 729 ikiwa nafasi ya 10 wakati Kinondoni ya Dar Es Salaam imeburuza mkia kwa kupoteza michezo yote 10 ikifungwa magoli 794 na kufunga magoli 188.CHANZO/MTANDA BLOG

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: