BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAAJABU YA SOKA NDIYO HAYA: TIMU YAFUNGWA KWA BAO 1-0 KATIKA FAINALI LAKINI NDIO BINGWA

Klabu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini imeshinda Kombe la Klabu Bingwa Afrika kwa mara ya kwanza baada ya kuwalaza Zamalek wa Misri kwa jumla ya mabao 3-1 kwenye fainali.

Kwenye mechi ya marudiano ya fainali mjini Alexandria, Zamalek walipata ushindi wa 1-0 Jumapili lakini haukutosha kwani walikuwa wamelazwa 3-0 na Sundowns mechi ya kwanza mjini Atteridgeville Jumamosi wiki iliyopita.

Hii ni mara ya kwanza kwa klabu hiyo ya Afrika Kusini kushinda kombe hilo.

Mara yao ya mwisho kufika fainali ilikuwa mwaka 2001 walipolazwa na mahasimu wakuu wa Zamalek, Al Ahly.

Zamalek walipata bao lao la pekee Jumapili dakika ya 62 kupitia Stanley Ohawuchi.

Kipa wa Sundowns Denis Onyango aliumia kwenye goti dakika ya 12 na akaondolewa uwanjani kwa machela dakika ya 28. Wayne Sandilands alichukua nafasi yake.

Maafisa wa Misri, ambao awali walikuwa wamesema ni mashabiki 20,000 pekee wangeruhusiwa uwanja wa Borg El Arab kwa sababu za kiusalama walibadilisha msimamo wao na kuruhusu theluthi tatu ya viti kwenye uwanja huo unaotoshea mashabiki 86,000 kujazwa.BBC
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: