BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MKOA WA MOROGORO CHASITISHA KUANDIKA HABARI ZA KIPOLISI IKIWEMO NA KUTOA TAMKO KUFUATIA KIFO CHA MWANDISHI CHANEL TEN MKOA WA IRINGA, DAUD MWANGOSI ALIYEFARIKI WAKATI WA RUVUGU BAINA YA POLISI NA CHADEMA NYOLOLO MUFINDI.


MWENYEKITI WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI MOROGORO, AZIZ MSUYA.
NA LILIAN LUCAS, MOROGORO. 
CHAMA cha waandishi wa habari mkoa wa Morogoro MOPC Kimesitisha kuandika habari za zozozte za polisi hadi pale baraza la habari MCT, Muungano wa Clabu za waandishi wa habari UTPC  na Jukwaa la wahariri watakapotoa tamko rasmi juu  ya mauaji ya  mwandishi wa habari wa kituo cha televisheni cha Chanel 10  Daud Mwangosi  yaliyosababishwa na polisi wakati mwangosi akiwajibika kazini katika mkutano wa Chadema.
Mwenyekiti wa MOPC  Aziz Msuya alisema hayo jana wakati wa mkutano wa pamoja na waandishi wa habari mjini Morogoro wenye lengo la kutoa tamko dhidi ya mauaji hayo.
Msuya alisema kuwa MOROPC inaungana na Clabu zingine za waandishi wa habari nchini katika kulaani vikali mauaji hayo yasio na hatia kwa mwandishi huyo na kwamba tukio kama hilo linaweza kumkumba mwandishi yeyote hivyo inasatahili kulipinga nwa nguvu zote.
‘’ Mauaji hayo hayana msingi wowote kwa mwanataalumu huyo ambaye alikuwa akiwajibika ili kuhakikisha wananchi wanapata haki yao ya habari sasa kama waandishi wasipolipinga hilo litazidi kutokea kwa siku za usoni.
Alisema kuwa kwa kuwa vyombo hivyo ambavyo  vinahusika moja kwa moja na waandishi wa habari vinatarajia kutoa tamko juu ya kifo hicho MOROPC imeamua kusitisha habari za polisi ili kusubiri tamko hilo.
Alisema kuwa ifahamike wazi kuwa kazi ya polisi ni kulinda mali  usalama wa watu na mali zao na sio kuuwa kama walivyoamua sasa kujichukulia sheria mkononi.

Alisema kuwa hali hiyo inatishia na kudhoofisha utendaji kazi wa waandishi wa habari na kuwafanya kuwa na woga  na hivyo kuonyesha dhairi kukiukwa kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini.
Kwa upande wake katibu wa chama hicho Abed Dogoli alisema kuwa MOROPC imeandaa utaratibu wa kupeleka rambirambi kwa familia ya marehemu huyo kama ilivyokuwa kawaida kwa wanataaluma hiyo kuungana pamoja wakati wa shida na raha.
Aliwataka Familia ya marehemu kuwa na subira kwa kipindi hiki cha majonzi ili kuweza kukamilisha uchunguzi wa tukio hilo ambalo bado linautata ndani yake.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: