BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WAHAMIAJI HARAMU 58 WAFARIKI DUNIA KATIKA AJALI YA MALI NCHINI UTURUKI

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/a701f860db923d9b90f43113bc378f61_XL.jpgAJALI ya boti iliyotokea leo katika eneo la Ahmetbeyli nchini Uturuki imesababisha vifo vya watu 58.

Boti hiyo ilikuwa imebeba wahajiri haramu wasiopungua 100 na ilizama baada kugonga mwamba ilipokuwa ikikaribia bandari ya magharibi ya Ahmetbeyli. 

Wengi wa wahajiri hao walikuwa kutoka nchi za Kiarabu. Baadhi ya manusura wamesema kuwa lengo lao lilikuwa ni  kufika Uturuki kisha kutumia njia za mkato kuingia barani Ulaya. 

Zaidi ya watu 40 wameokolewa kwenye ajali hiyo. 

Makumi ya maelfu ya wahajiri haramu hufa maji kila mwaka wakijaribu kuingia Ulaya kupitia Uturuki na Libya na wengine hupoteza maisha baharini wakijaribu kuingia Australia. 

Baadhi ya nchi za Ulaya zimeweka sheria kali ili kukabiliana na ongezeko la wahajiri haramu.

Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: