BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

CHAMA TAWALA ANGOLA CHASHINDA UCHAGUZI MKUU


Bild: António Cascais
Wann wurde das Bild gemacht?: 31.08.12
Wo wurde das Bild aufgenommen?: Luanda, Angola
CHAMA tawala nchini Angola cha MPLA chini ya rais Jose eduardo dos Santos kimetangazwa rasmi kuwa kimeshinda uchaguzi wa bunge la nchi hiyo uliofanyika Ijumaa iliyopita. 

Vyombo vya habari vya serikali vilitangaza taarifa hiyo hata kabla ya matokeo ya mwisho kutolewa. 

Kwa hivyo, rais dos Santos anabakia miaka mitano zaidi madarakani.

Wapiga kura wa Angola wakisubiri kushiriki uchaguzi mjini Luanda
Wapiga kura wa Angola wakisubiri kushiriki uchaguzi mjini Luanda.

Kutokana na mabadiliko ya katiba ya mwaka 2010 ni kwamba kiongozi wa chama kilichopata kura nyingi kabisa anakuwa rais na mkuu wa serikali.  

Taarifa za Tume ya Uchaguzi iliyotangazwa katika mji mkuu wa Luanda ilitaja kwamba asilimia 75 ya wapiga kura walikichagua chama cha MPLA.

Chama kikubwa kabisa cha upinzani, UNITA, kilipata asilimia 18 ya kura. Msemaji wa upinzani na waangalizi huru wa uchaguzi hapo kabla walilalamika kwamba kulikuweko kasoro katika zoezi la uchaguzi huo. Jumla ya viti 220 vimeshindaniwa katika uchaguzi huo.

Uchaguzi umekwenda kwa amani.
Mamlaka nchini humo imesema kuwa zoezi la upigaji kura limefanyika kwa amani. 

Huu ni uchaguzi wa tatu nchini Angola tangu ipate uhuru wake kutoka kwa Wareno mwaka 1975. Uchaguzi wa mwisho ulifanyika mwaka 2008.

Kituo cha kupigia kura Angola
Kituo cha kupigia kura Angola.

Uchaguzi uliotangulia kabla ya huo wa mwaka 2008 ulifanyika mwaka 1992. Matokeo ya kutatanisha ya uchaguzi huo yalizusha awamu ya pili vya vita vya muda mrefu vya wenyewe kwa wenyewe katika taifa hilo la kusini mwa Afrika.

Katika uchaguzi wa safari hii, kwa mara ya kwanza Waangola walioko nje wanaoishi nchini Ureno wamekataliwa kupiaga kura.
José Eduardo dos Santos, Rais wa  Angola
José Eduardo dos Santos, Rais wa Angola.

Angola imepata mafanikio kiuchumi kutokana na mafuta. Hata hivyo wachambuzi wameonya kuwa wakati wasomi wachache wananufaika, kundi kubwa la raia wameendelea kubaki katika dimbwi la umasikini.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: