BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

IMAM KHAMENEI ATAKA WALIOMTUSI MTUME MUHAMADI (SAW) WAADHIBIWE

Imam Khamenei: Waliomtusi Mtume waadhibiwe Imam Khamenei

 KUATIA kitendo cha maadui wa Uislamu cha kumvunjia heshima Mtume Mtukufu Muhammad SAW, Ayatullah Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametoa ujumbe kwa taifa la Iran na umma mkubwa wa Kiislamu akisema kuwa, siasa za kihasama za Wazayuni, Marekani na vinara wengine wa ubeberu wa kimataifa ndizo zilizohusika na harakati hiyo iliyojaa shari.

Ameweka wazi sababu za kinyongo cha Wazayuni dhidi ya Uislamu na Qur'ani na akasisitiza kuwa, kama wanasiasa wa Marekani wanasema kweli katika madai yao kwamba hawakuhusika katika jinai hii, basi wanapaswa kuwapa adhabu inayonasibiana na jinai hii wale wote waliohusika na uhalifu huo mkubwa na waliowasaidia kifedha ambao wamezitia simanzi na maumivu nyoyo za mataifa ya Waislamu.

Ayatullah Khamenei amesema lau kama mabeberu wa kimataifa wasingeunga mkono sehemu za kwanza za mnyororo huu muovu yaani Salman Rushdie, mchora vikatuni wa Denmark na makasisi wa Kimarekani waliochoma moto Qur'ani, na kuacha kuagiza makumi ya filamu zinazopiga vita Uislamu kutoka kwenye makampuni ya wawekezaji wa Kizayuni basi hali isingefikia kiwango hiki cha kutenda dhambi kubwa na isiyosameheka.

Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Waislamu kote duniani wanapaswa kuelewa kwamba, harakati hizi zilizofeli za maadui dhidi ya mwamko wa Kiislamu ni kielelezo cha adhama na umuhimu wa mwamko huo na bishara ya kustawi kwake zaidi.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: