BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE KATIKA SHIRIKISHO LA KIISLAM (OIC) KUKABILIANA NA VITENDO VYA DHARAU DHIDI YA MTUME MUHAMADI (SAW).

MAWAZIRI wa Mambo ya Nje wa nchi wanachama katika Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) watajadili njia za kukabiliana na vitendo vya dharau na kumvunjia heshima Mtume Muhammad (saw).

Balozi na mwakilishi wa Iran katika Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) Hamid Reza Dahqani amesema kuwa mawaziri hao watajadili njia za kukabiliana na dharau na vitendo vya kuyavunjia heshima matukufu ya Kiislamu katika mkutano wao wa 39 utakaofanyika nchini Djibouti na ule utakaofanyika katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York.

Ameashiria mikono ya nyuma ya pazia iliyohusika katika kuvunjia heshima matukufu ya Kiislamu na kusema kuwa, Wamagharibi daima wamekuwa wakidai kuwa masuala hayo yanatokana na uhuru wa kusema na kujieleza katika katiba za nchi zao.

 Dahqani ameongeza kuwa taasisi za kimataifa zinasisitiza juu ya udharura wa kuheshimiwa dini za mbinguni, thamani na itikadi za mataifa mbalimbali lakini inasikitisha kuwa hadi sasa juhudi za jumuiya za kutetea haki za binadamu na jumuiya za kimataifa ikiwemo OIC hazijafanikiwa kuwakinaisha Wamagharibi kuhusun ukweli kwamba uhuru hauna maana ya kuvunjia heshima matukufu ya itikadi za watu wengine.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: