BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

WATU 45 WAFARIKI DUNIA KATIKA MAPIGANO NCHINI SOMALIA.


WATU wasiopungua 45 wameuawa na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa katika mapigano yaliyotokea kusini mwa kijiji cha Bibi kati ya majeshi ya Kenya na Somalia kwa upande mmoja dhidi ya wapiganaji wa kundi la al Shabaab.

Mapigano hayo yametajwa kuwa ndiyo makali zaidi kutokea huko kusini mwa Somalia tangu majeshi ya Kenya yaingie nchini humo mwezi Oktoba mwaka jana.

Mapigano baina ya pande hizo mbili yalishadidi zaidi baada ya jaribio la majeshi ya Kenya na Somalia la kutaka kuingia katika ngome za kundi la al Shabaab karibu na kijiji cha Bibi.

Hadi sasa hakujatolewa habari kamili kuhusu idadi kamili ya watu waliouwa katika mapigano hayo kutoka pande zote mbili lakini vyombo vya kuaminika vinasema makumi ya watu wameuawa.

Duru za kundi la al Shabaab zinasema kuwa ndege za kijeshi za Kenya zinashiriki katika mapigani hayo makali.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: