BannerFans.com

MBUNGE SUZAN KIWANGA AKWAMISHA KESI MAHAKAMANI MOROGORO

BARAZA LA USALAMA LAWAWEKEA VIKWAZO WAASI WA M23 DRC.

 http://gdb.voanews.eu/FD706CE3-B043-4FBB-88E1-9C0D17438121_mw1024_mh768_s.jpg
BARAZA la Usalama la Umoja wa Mataifa limewawekea vikwazo waasi wa M23 wa Kongo DRC baada ya waasi hao kudhibiti mji wa Goma ambao ni makao makuu ya mkoa wa Kivu Kaskazini hapo jana. 

Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema, viongozi wa waasi wa M23 wanawekewa vikwazo kwa mujibu wa azimio la Umoja wa Mataifa na kutaka kukomeshwa uungaji mkono wa nchi za nje kwa waasi hao.
http://gdb.voanews.eu/2F70115D-16C4-41D2-9459-FD374277E9EE_mw1024_mh768_s.jpg
 Hayo yanajiri huku waasi wa M23 wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda na Uganda wakitangaza kwamba wana mpango wa kukomboa nchi nzima ya Kongo DRC baada ya kudhibiti mji wa Goma. Vilevile maelfu ya askari na polisi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameasi serikali na kujiunga na waasi wa M23 katika mji wa Goma. 
http://gdb.voanews.eu/AA31A68F-5178-478F-BB25-2D37C356CE6A_mw1024_mh768_s.jpg
Taarifa zinasema kuwa askari hao waliojiunga na jeshi hawakuwa na khiyari baada ya waasi hao kuwalazimisha kujiunga na kundi hilo na kuwataka ima kubakia kwenye mji huo au kuondoka. 

Msemaji wa waasi hao amesema kuwa, kundi hilo lina mpango wa kudhibiti nchi nzima ya Kongo kwa kuanza kuelekea katika mji wa Bukavu hadi katika mji mkuu Kinshasa, ulioko umbali wa kilometa 1,600 kutoka Goma.
Share on Google Plus

About mtanda blog

Blogger maarufu nchini Tanzania na mwanahabari mkongwe kwenye Tasnia ya habari
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: